Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ADA-TADEA, Ally Makame, ameikosoa vikali kauli ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ya No Reforms, No Election, akidai kuwa ni jaribio la kujipa mamlaka ya kipekee kisiasa na kupotosha mwelekeo wa taifa kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
Akizungumza katika mahojiano na Wilberforce Ngoto wa Jambo TV kupitia kipindi cha Maswali na Majibu, Makame amesema kuwa madai ya CHADEMA kwamba ni lazima kufanyike mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi kabla ya kushiriki uchaguzi ni ya kibeberu na hayana msingi wa kidemokrasia.
Makame ameeleza kuwa hali ya sasa ya kisiasa nchini ni tulivu, na kwamba uchaguzi ujao unatarajiwa kufanyika kwa amani na utulivu bila masharti ya kisiasa yasiyo ya lazima.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vyama vyote kwenye mchakato wa uchaguzi, Makame amesema kuwa mageuzi ya kisiasa ni muhimu lakini hayawezi kuwa kisingizio cha kugomea chaguzi.
Akizungumza katika mahojiano na Wilberforce Ngoto wa Jambo TV kupitia kipindi cha Maswali na Majibu, Makame amesema kuwa madai ya CHADEMA kwamba ni lazima kufanyike mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi kabla ya kushiriki uchaguzi ni ya kibeberu na hayana msingi wa kidemokrasia.
Makame ameeleza kuwa hali ya sasa ya kisiasa nchini ni tulivu, na kwamba uchaguzi ujao unatarajiwa kufanyika kwa amani na utulivu bila masharti ya kisiasa yasiyo ya lazima.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vyama vyote kwenye mchakato wa uchaguzi, Makame amesema kuwa mageuzi ya kisiasa ni muhimu lakini hayawezi kuwa kisingizio cha kugomea chaguzi.