Aliyoyasema Tundu Lissu yatimia!

Aliyoyasema Tundu Lissu yatimia!

Nawashangaa wachangiaji wnaoikataa hoja ya Lissu. Hebu mjipe kanafasi ka dogo hivi muisome katiba yenye viraka vingi ya mwaka 1977 mjiridhishe kabla ya kuchangia kiushabiki. Au nanyi ni wa buku 7 wenye kujibu hoja pasi na kuwa na hoja? Ndo maana mnaburuzwa as if nchi hii ni ya kifalme. Wameweka sheria lazima wazizinagatie na kuzitii. Hongera Lissu kwa kuwakumbusha hawa wavivu wa kusoma japo vitu vidogo kama katiba. Nawaasa m-badilike kwani wasomi wa aina yenu hamna manufaa kwa taifa lenu na mnachangia umaskini kwa wananchi waliojtolea kodi zao ili msome. Laiti wanangalijua mtakuja kuwa hivi wangegoma kulipa kodi ili mkachunge ng'ombe!
 
Tundu lissu ni mgonjwa wa kudumu mirembe

Jikite kwenye hoja. Kwani lowasa anaendeaga nn ujerumani. Tezi dume ni nn? Aliugua Nani..
Tusijadili mapungufu ya mtu, Bali tujadili hoja yake. Ndio maana ya jukwaa. Hakuna aliyetimia.
 
Mahakama zipo wakapinge mahakamani sheria zipekuliwe.

1434805285899.jpg Hata hii inahitaji mahakama gani kufafanua jamani?
 
Augustino ramadhani akiteuliwa na ccm kugombea urais atawekewa pingamizi la kikatiba. uzuri wake naye ni mwansheria anajua hilo

Akili za Kawaida haziamini kama Pingamizi hilo litasababisha Augustino Ramadhani aondolewe kupeperusha Bendera ya CCM kama Mgombea wake wa Kiti cha Urais.
 
Hutu tundu lisu tangu ahamasishe migawanyiko na kufukuzana ndani ya cdm na kuitwa kifaranga,nilimdharau toka Siku hiyo.
 
Huyo kisha staafu kumbe out haimuhusu ukwenda shule

katiba ya ccm inasema "kugombea urais kupitia chama cha mapinduzi hadi uwe mwanachama hai kwa kipindi kisichopungua miaka mitano" je jaji huyu tangu astaafu ana muda gani?
 
Augustino ramadhani akiteuliwa na ccm kugombea urais atawekewa pingamizi la kikatiba. uzuri wake naye ni mwansheria anajua hilo

Hawa nı team Edo tu wala si UKAWA.Leo mnamquote Lısu??Kimsıngi hakuna katiba ya nchi yoyote itakayoweka kifungu cha kuzuia mtumishi yeyote asigombee nafasi ya Urais kwani utumishi wowote ni moja ya vitu vınavyomjengo kiongozı.La msıngi akiamua kwenda kule anaacha huku.Na ikitokea basi huyo mtu itabidı ahudumiwe na jamii maisha yake yote tena kwa kiwango cha juu.
 
Huyu mwandishi ametimiza wajibu wake kwa umma ni juu yetu wananchi sasa kupima uadifu wa huyu jaji.

Ningekuwa mwenye maamuzi UKAWA, ningefanya kuwaacha CCM waendelee na utaratibu wao wa chama, kisha nafungua kesi ya pingamizi dhidi ya aliye teuliwa mfn huyo Jaji. Au naye atakuwa kama Mwizi- Nyoka makengeza asiye chunguzwa? Hizi makama nazo, hata hawawaliobaki watasema hawana mamlaka ya kumchunguza aliye wahi kuwa mkuu wao…… Tanzania…. Ikipata watu wabunifu tunaweza kupata watalii wengi wa kuja kushangaa maajabu ya Tanzania!!!!
 
Mkuu mbona unacheka la ajabu lipi? kwani tundu lisu ye nani asidharauliwe ?
Hivi yuko mwanadamu anayestahili kudharauliwa? La hasha hakuna hata mmoja sababu wanadamu wote ni sawa kwa sababu mbili kuu: kwanza; Wote wameumbwa na Mungu kwa mfano wa Mungu. Pili; wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu na hivyo kuhitaji neema ya Bwana.

Wewe una utakatifu gani unaokupa haki ya kudharau wengine wakati hata Mungu hadharau viumbe wake?

Hupaswi kumdharau Lissu lakini ni ruksa kupinga hoja yake kwa kutoa hoja mbadala. Inawezekana hata katiba ya 1977 hujawahi kuiona, wawezaje kumdharau au hata kumpinga Lissu?
 
Nyota ya mwaka huu ni UKAWA tu, kwani miaka 54 ya utawala wa mfumo huo huo mmoja sasa inatosha. Tumedanganywa sana na sasa tunasema imetosha. Wengi wetu tuko tayari sasa kujaribu plan B na tuna uhakika Bahari ya Sham tutavushwa kwa usalama wa kutosha na mtu yeyote kutoka nje ya Chukua Chako Mapema (CCM). Tusubiri 25.10.2015 na hili litawezekana tu kama kutakuwa na fair play kwenye zoezi zima la uchaguzi kuanzia kujiandikisha hadi kupiga kura kwa mfumo mpya BVR.
 
Huyu mwandishi ametimiza wajibu wake kwa umma ni juu yetu wananchi sasa kupima uadifu wa huyu jaji.

Una shaka gani na uadilifu wa mwadilifu mchungaji Augustine Ramadhan?yeye ni mstaafu sana hivyo habanwi na sheria hiyo, mngetaka mngemuomba ata agombee kupitia chadema maana kwa CCM tunao wengi wenye sifa ila kwenu huko hakuna mwenye sifa ata walau robo ya zile za Jaji huyu.
 
Back
Top Bottom