Aliyekuwa Kamanda Mkuu wa Ulinzi wa Kagame ahukumiwa miaka 21 jela

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,880
6,367
Aliyekuwa kamanda mkuu wa kikosi cha ulinzi wa Rais Paul Kagame, Kanali Tom Byabagamba, amehukumiwa kifungo cha miaka 21 jela na kuvuliwa cheo chake baada ya kupatikana na hatia ya kuharibia sifa nchi hiyo na kuhamasisha wananchi kupinga utawala.

Kesi hiyo ilimhusisha pia brigedia jenerali mstaafu Frank Rusagara ambaye naye amepatikana na hatia na kuhukumiwa miaka 20 jela.

Maafisa hao wa jeshi wamepinga hukumu hiyo wakisema mashtaka dhidi yao yalichochewa kisiasa.

Mahakama imeunga mkono hoja za upande wa mwendesha mashtaka kwamba mlinzi wa muda mrefu wa Rais Kagame, Kanali Byabagamba, alihusika na makosa matatu ambayo ni kueneza kampeni za chuki dhidi ya utawala ambazo zingesababisha wananchi kugoma dhidi ya serikali ya nchi hiyo na kutoheshimu bendera ya nchi hiyo.

Brigedia jenerali mstaafu Frank Rusagara naye amepatikana na makosa kama hayo pamoja na kosa la kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Awali alikiri kumiliki bastola mbili alizopewa kama zawadi na nchi za Afrika Kusini na Israel, wakati alipokuwa afisa mkuu anayehusika na ununuzi wa silaha katika wizara ya ulinzi ya Rwanda.

Maafisa hao wamekata rufaa baada ya mahakama kutangaza hukumu hiyo.


Chanzo: BBC
 
Hapo labda alitaka kugombea nafasi ya ufalme.Hakujua hicho kiti mpaka aingie kaburini
 
ImageUploadedByJamiiForums1459541877.277547.jpg
Walitoka mbali
 
Aliyekuwa kamanda mkuu wa kikosi cha ulinzi wa Rais Paul Kagame, Kanali Tom Byabagamba, amehukumiwa kifungo cha miaka 21 jela na kuvuliwa cheo chake baada ya kupatikana na hatia ya kuharibia sifa nchi hiyo na kuhamasisha wananchi kupinga utawala.

Kesi hiyo ilimhusisha pia brigedia jenerali mstaafu Frank Rusagara ambaye naye amepatikana na hatia na kuhukumiwa miaka 20 jela.

Maafisa hao wa jeshi wamepinga hukumu hiyo wakisema mashtaka dhidi yao yalichochewa kisiasa.

Mahakama imeunga mkono hoja za upande wa mwendesha mashtaka kwamba mlinzi wa muda mrefu wa Rais Kagame, Kanali Byabagamba, alihusika na makosa matatu ambayo ni kueneza kampeni za chuki dhidi ya utawala ambazo zingesababisha wananchi kugoma dhidi ya serikali ya nchi hiyo na kutoheshimu bendera ya nchi hiyo.

Brigedia jenerali mstaafu Frank Rusagara naye amepatikana na makosa kama hayo pamoja na kosa la kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Awali alikiri kumiliki bastola mbili alizopewa kama zawadi na nchi za Afrika Kusini na Israel, wakati alipokuwa afisa mkuu anayehusika na ununuzi wa silaha katika wizara ya ulinzi ya Rwanda.

Maafisa hao wamekata rufaa baada ya mahakama kutangaza hukumu hiyo.


Chanzo: BBC
Huyo Ndio Kagame!!! Akikuchoka anakutengenezea kesi then unapata long incarceration!!!!
 
Back
Top Bottom