Dogo atakuwa anakula tu mafao yake. Mzigo wa bilioni 1+ uliingia kwenye akaunti yake ya NMB! Baada ya gharama za kuwalipa mawakili wake na tozo za hapa na pale, lazima tu atakuwa amelaza milioni 800-900 hivi.
Sasa akiamua kuwekeza hiyo hela kujengea nyumba za wageni na zile za kuoangisha kwenye maeneo mazuri; hapo kila mwezi unakusanya tu kodi maisha yako yote. Hakika Tp Mazembe watakuwa mpaka sasa wanajutia sana kumfahamu huyu dogo.