Makonyeza
Member
- Feb 2, 2020
- 69
- 252
Spotpesa na Dar Young Africa, akili kubwa sana.
Wala haihitaji nguvu nyingi akili ikijitosheleza. Maana mantiki na malengo ya matangazo ya biashara ni jamii au umma unaolengwa kama walaji wa huduma ya Kampuni husika kuijua kampuni yao na huduma zake.
Ndiyo sababu watu maarufu wenye kujitambua wakihojiwa huzuia kuonesha bidhaa za kampuni kama nembo za vinywaji au mavazi ambazo hana mkataba nazo.
Spotpesa ndio wadhamini wakuu wa Club ya Yanga na kwa ajili hiyo popote Yanga ikionekana Jina la mdhamini huyu litatakiwa kuonekana kifuani kwenye vazi la mwana Yanga. Lile lengo la kuitangaza kwa umma linatimia na ndio Uhai wa Kampuni.
Kanuni za ushiriki wa Yanga au timu yoyote mashindano ya Caf hairuhusu kuvaa nembo ya Kampuni ya Kamali, yaani Bet kwa sababu na wao wanadhaminiwa na kampuni ya Kamali.
SPOTPESA ni mhanga wa kanuni hii na anajua hali ilivyo, afisa mahusiano wa Kampuni hiyo amethibitisha. Kwa hiyo wala usitegemee au kutarajia spotpesa kunufaika na mashindano yoyote ya Caf.
Sasa ili wanufaike inahitajika akili ya ziada, ndicho kilichofanyika. Yanga Katangaza mdhamini mpya kwa mashindano ya Caf, Haier.
Eng. said amethibitisha walishauriana na wadhamini wao wakuu, na afisa mahusiano wa SPOTPESA amethibitisha hilo, lakini wakati Huohuo taharuki inaibuka SPOTPESA wanadaiwa kulalamika kwamba hawa kutoa ridhaa hiyo.
Sasa matokeo au athari yake ni kama unavyoona, kila redio na magazeti kwa wiki nzima Sasa wanajadili (kuitaja) spotpesa. Kiufundi lengo limetimia, Spotpesa Inatangazwa na Vyombo vya habari bila kulipia, na ndio wamenufaika na mashindano ya Caf kwa kutumia akili.
Ukiwa Dunduka huwezi kuyaelewa haya.
Wala haihitaji nguvu nyingi akili ikijitosheleza. Maana mantiki na malengo ya matangazo ya biashara ni jamii au umma unaolengwa kama walaji wa huduma ya Kampuni husika kuijua kampuni yao na huduma zake.
Ndiyo sababu watu maarufu wenye kujitambua wakihojiwa huzuia kuonesha bidhaa za kampuni kama nembo za vinywaji au mavazi ambazo hana mkataba nazo.
Spotpesa ndio wadhamini wakuu wa Club ya Yanga na kwa ajili hiyo popote Yanga ikionekana Jina la mdhamini huyu litatakiwa kuonekana kifuani kwenye vazi la mwana Yanga. Lile lengo la kuitangaza kwa umma linatimia na ndio Uhai wa Kampuni.
Kanuni za ushiriki wa Yanga au timu yoyote mashindano ya Caf hairuhusu kuvaa nembo ya Kampuni ya Kamali, yaani Bet kwa sababu na wao wanadhaminiwa na kampuni ya Kamali.
SPOTPESA ni mhanga wa kanuni hii na anajua hali ilivyo, afisa mahusiano wa Kampuni hiyo amethibitisha. Kwa hiyo wala usitegemee au kutarajia spotpesa kunufaika na mashindano yoyote ya Caf.
Sasa ili wanufaike inahitajika akili ya ziada, ndicho kilichofanyika. Yanga Katangaza mdhamini mpya kwa mashindano ya Caf, Haier.
Eng. said amethibitisha walishauriana na wadhamini wao wakuu, na afisa mahusiano wa SPOTPESA amethibitisha hilo, lakini wakati Huohuo taharuki inaibuka SPOTPESA wanadaiwa kulalamika kwamba hawa kutoa ridhaa hiyo.
Sasa matokeo au athari yake ni kama unavyoona, kila redio na magazeti kwa wiki nzima Sasa wanajadili (kuitaja) spotpesa. Kiufundi lengo limetimia, Spotpesa Inatangazwa na Vyombo vya habari bila kulipia, na ndio wamenufaika na mashindano ya Caf kwa kutumia akili.
Ukiwa Dunduka huwezi kuyaelewa haya.