Zingatia yafuatayo:
1. Muwe na shughuli ya kiuchumi
2. Kama hamzidi watu 20
3. Sajili jina la kikundi chenu brela
4. Andaeni muhtasari wa kikao cha makubaliano ya kikundi chenu ambapo kila mjumbe atatia sahihi.
5. Kikundi kiwe na viongozi- Mkiti, Katibu, Mhazini
6.Andikeni kwa Meneja wa Benk kuomba kufungua akaunti ya kikundi
6. Sema watia sahihi benki, na namna watakavyoweza kutoa pesa.
7. Ambatanisha nyaraka tajwa hapo juu, usajili, Tin, leseni.
Kazi rahisi, mwaweza kufanya wenyewe, kama mtahitaji msaada tuwasiliane ktk private box. Nawashauri mfungue akaunti Equity Bank Tanzania- hakuna mizegwe.