Ajali mbaya mabasi matano yagongana

Ajali mbaya mabasi matano yagongana

Status
Not open for further replies.

BIGURUBE

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2014
Posts
6,748
Reaction score
4,257
Kuna taarifa nimezipata kuna mabasi matano yaliyokuwa yakitokea Arusha yamegongana...mwenye habari kamili tunaomba updates

JAMIIFORUMS: Habari hii si ya kweli, ni ajali ya 2012 na ilihusisha mabasi ya simba mtoto na Dar express pia ilishawahi kuzushwa tena Septemba 2014


Uongozi wa Kampuni za Mabasi ya Dar Express na Simba Mtoto umefafanua kuwa hakuna ajali iliyotokea kama ilivyoripotiwa jana.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwapo taarifa za ajali eneo la Wami, Darajani ambazo zilidaiwa kuhusisha mabasi ya Dar Express na Simba Mtoto.

Ajali ya mabasi hayo iliwahi kutokea eneo hilo mwaka 2012, lakini si juzi kama ilivyoripotiwa.

Msemaji wa Polisi mkoa wa Pwani, Hassan Juma alisema juzi kuwa walipata taarifa za ajali na walikuwa wanakusanya taarifa zaidi.

Alipoulizwa Kamanda Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Pwani, Athumani Mwambalaswa jana asubuhi, alisema kuwa ofisi yake haina kumbukumbu za kutokea ajali kama hiyo.

Alipotafutwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Frassier Kashai jana, naye alisema kuwa hakuna kitu kama hicho.

Pamoja na kuwapo taarifa hizo, tumethibitisha pasi na shaka kuwa hazina ukweli. Tunaomba radhi kwa wote walioguswa au kupata usumbufu wa taarifa hiyo ambayo tuliichapisha jana katika gazeti hili-Mhariri.


CHANZO: Mwananchi(Septemba 10, 2014)
 

Attachments

  • 1420451173922.jpg
    1420451173922.jpg
    14 KB · Views: 378
  • 1420451191637.jpg
    1420451191637.jpg
    14.2 KB · Views: 341
  • 1420451208875.jpg
    1420451208875.jpg
    58.2 KB · Views: 339
  • 1420451224264.jpg
    1420451224264.jpg
    54.2 KB · Views: 343
Hata mimi nina wasiwasi na hii habari!
 
Ok wenye taarifa sahihi watujuze
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom