monaco
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 2,184
- 1,779
Katika maeneo baada kidogo ya nangulukulu Km1 hivi,basi likiwa kinatokea nangulukulu kuelekea Dsm lilikutana na Lori lililokuwa kimekaa katikati ya barabara kutoka Dsm kuja nangulukulu,dereva alipotaka kulikwepa akakutana na Lori lingine linakuja upande aliokuwepo,ikabidi arudi pembeni kuepusha ajali ya USO kwa USO,alipokuwa anarusisha gari njia kuu gari ikateleza ikagoma kurudi njia kuu ikateleza Kama linavyoonekana ktk picha!jamani haya malori haya!hakuna mtu aliepoteza Maisha kikubwa abiria wote walikuwa wamefunga Mkanda,mikanda imesaidia sana sana jamani!tulivyofika hapo tukawapa msaada wa kuwapakia baadhi ya abiria!wengine walipelekwa hospitali ya kilwa!