Ajali Barabarani Chanzo Kikuu ni Polisi?

Ajali Barabarani Chanzo Kikuu ni Polisi?

Edogan

Member
Joined
May 19, 2024
Posts
39
Reaction score
63
Hii nchi bwana haiishiwi vituko yani nikama kila sekta pana watu wasiokua na weledi na fani wanazozitumikia yani.

Pamoja nakua tunapokua shuleni na vyuoni tunakumbana na misemo nahau vitendawili methali na kadhalika lakini havitusaidii lolote. Kwamfano unaweza kushangazwa na Jeshi la Polisi kuwalaumu au kutishia kuwachukulia hatua kali Madereva wa magari endapo watasababisha ajali au watagundulika kutumia matumizi ya Barabara kwa kuvunja sheria

Ila wanasahau kua zaidi ya 80% ya madereva wa Tz hawajui sio tu kuendesha gari vizuri ila pia sheria za Barabarani. Na kwa kiasi kikubwa inachangiwa na haohao Polisi ambao hugawa Leseni za Udereva bila kuzingatia sheria.

Mtu anatoa hela unamuidhinisha akakate leseni wakati unajua hana mafunzo ya Udereva akipata ajali unamchukuliaje hatua?
 
mtu anatoa hela unamuidhinisha akakate leseni wakati unajua hana mafunzo ya Udreva
Siyo kwamba mtu anaidhinishwa, huwa askari polisi wanapewa hela (rushwa) halafu wao wenyewe wanampelekea leseni mtoa hela (rushwa).
 
Umeandika vema. Madereva wengi hawajui wanachokifanya. Imagine mtu unaendesha lori limebeba kontena ambalo limeegeshwa tu bila kufungwa kwenye trailer. How reckless is that?
 
Kingine huko barabarani vichaa wengi, ujuaji mwingi

Ova
 
Hii nchi bwana haiishiwi vituko yani nikama kila secta pana watu wasiokua na weledi na fani wanazozitumikia yani pamoja nakua tunapokua shuleni na vyuoni tunakumbana na misemo nahau vitendawili methali na kadharika lakini havitusaidii lolote, kwamfano unaweza kushangazwa na Jeshi la Polisi kuwalaumu au kutishia kuwachukulia hatua kali Madreva wa magari endapo watasababisha ajali au watagundulika kutumia matumizi ya Barabara kwa kuvunja shelia, ila wanasahau kua zaidi ya 80% ya madreva wa Tz hawajui sio tu kuendesha gali vizuli ila pia shelia za Barabarani, Na kwa kiasi kikubwa inachangiwa na haohao Polisi ambao hugawa Leseni za Udreva bila kuzingatia sheria, mtu anatoa hela unamuidhinisha akakate leseni wakati unajua hana mafunzo ya Udreva akipata ajali unamchukuliaje hatua?
Hili la kugawa leseni nadhani unazungumzia utaratibu wa siku za nyuma; nenda ka renew leseni yako sasa hvi uone, hauna cheti hupati leseni; cheti chako kikiwa kidogo, utapewa daraja la chini.
Madereva wengi wa Tanzania hasa wanao sababisha ajali, tatizo sio competency wala police, tatizo kubwa ni dharau na kutokujali. Wabongo wengi (nje ya Madereva) hatunaga historia ya kujali vitu vya watu. Mtu anajua, eneo hili, haruhusiwi ku overtake but anafanya hivo, sometimes wana overtake akiwa hajui mwenzie wa mbele why ka slow down, mwisho anakwenda anagonga.
Tazama gari za serikali kwamfano, hata kwenye maeneo yenye population kubwa, wao ni speed tu, utasema Madereva wale nao hawana ujuzi? La hasha, wale wana VIP Driving skills kabisa, but angalia nidhamu zao wawapo barabarani. Police/traffic tunawatwisha dhambi nyingi, kwa hili HAPANA.
 
Back
Top Bottom