Ajae ni mwana Singida Mashariki kweli?

Ajae ni mwana Singida Mashariki kweli?

KAYABOMBICHI

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2013
Posts
296
Reaction score
142
Tume ya Taifa imetangaza tarehe ya uchaguzi jimbo la Singida Mashariki jimbo ambalo mbunge wake yuko hai anapambania uhai wake hospitalini.

Ubelgiji najua wananchi wa Singida Mashariki walikuwa wakimsubiri kwa hamu mbunge wao aje awaeleze nini kilichompata lkn ghafla ndo hiyo imezimwa na sasa wanaandaliwa mbunge mpya!!

Najiuliza ni nana huyo mwenye roho ngumu kiasi hicho,ni mwana singida mashariki kweli asiye hata na chembe ya uoga wala aibu ?Atasimama jukwaa lipi?

Atawaeleza nini wanasingida mashariki?

Inahitaji akili ya ziada kuukubali ubunge huo kwa mazingira haya !
 
Nasikitika nilisikia tetesi CCM wanamtaka Dr. John Jingu. Huyu jamaa ni mtu safi sana, namjua vizuri...lakini watamuweka pabaya maana huko nyumbani watu wanamlilia Lissu kwa majanga aliyopata..ije mtu ukawaombe kura mara hii, tena kwa kumkandia Lissu.

Dr. Jingu please usibebeshwe mzigo huu...ww ni muungwana sana ndugu yangu.
 
Hiyo atakayegombea. Ubunge huko ajiandae kwa chochote huenda hats asifike 2020. Mungu hadhihakiwi
 
Sijui watanzania tumemkosea nini Mungu ? Mpaka shetani akaamua kushuka kabisa Tanzania kupitia ccm kuteletea mateso ,dhiki ,ufukara ,umaskini ,balaa ,nuksi ,maisha magumu na laana zote za duniani kwa muda mfupi tu .
 
Wengi mnahurumia kukosa kiti kwa Tundu Lissu, mnaumia Chadema kupunguza mbunge Bungeni huku CCM wakishangilia ujinga wa kuwaweza Chadema kwa ujanja huo
Ila mtu ambaye ni mwenye maono ya Mbali hawezi umia Lissu kukosa ubunge, wala Chadema kupunguza ubunge, ila Ataumia juu ya kitendo cha kumiminiwa risasi mheshimiwa Lissu,

Pia wapumbavu watashangilia kuwa wamempunguza nguvu ya, chadema Bungeni,

Lakin mwelevu kama kuna la Kufurahia ni miujiza ya Mungu iliyomfanya Lissu aendelee kuwa hai,

Vyeo ni ishu ndogo za kuacha duniani,

Britannica
 
Back
Top Bottom