Airtel Tanzania, huu ni wizi

Airtel Tanzania, huu ni wizi

boyayoparuparu

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2015
Posts
343
Reaction score
82
Hawa Airtel Tanzania, ni kampuni nyonyaji kwenye tangazo lao linalo endelelea siku hizi wanasema wanajali pesa za wanao tumia huduma ya airtel money, kwa ujumla eti wanajali pesa ya mteja, jambo ambalo sio kweli.

Hebu fikiria unapo wapigia simu kuwaambia tatizo flani lililojitokeza, kwanza simu inaita muda mrefu huku ukiambiwa kuwa usubiri utapokelewa baada ya muda mrefu ukipata bahati ya kupokelewa, unaanza unaeleza tatizo mara simu inakatika.

Wakati mwingine unakuwa bado haujapatiwa ufumbuzi wa suala lako, ukipiga tena unaambiwa simu yako itakatwa sh sitini, hizo sh sitini mnazozikakata ni kwaajili gani, hivi mtu ukuwa na land line ukawa na exintantion chumbani, unapotaka kupiga simu sebuleni ukiwa chumbani unailipia?

Acheni dhuluma hii, shida zinazo tokea tunapoziwasilisha kwenu nikwa faida yenu iweje tena mtutoze pesa.
 
Yaan hawa wanakiburi sana... Wanafikirije cjui... Nway cku itafika 2taishi bila dhuluma...
 
Naanza kuelewa kuwa matatizo yapo tcra,wao ndio wangekuwa wakwanza kugundua dhuluma lakini ndio hivyo tena
 
Airtel imeniliza jana. Nimejiunga na kifurushi cha 500 (Dak 18 Airtel-Airtel) na 500 (Dak 9 Airtel-Any network). Nimejiunga saa mbili usiku nikijua nitakapoamka asubuhi niwasiliane na watu, cha ajabu sijakuta kitu kwenye simu. Elfu moja yangu imeniuma sana bora ningeidondosha njiani huko kuliko kuliwa namna hiyo. Airtel pumbavu zenu pamoja na watoa huduma wote pumbavu, na mtandao wenu pumbavu zenu na mkurugenzi wenu pumbavu zake!!. Mnatuua mnatusababishia ugumu wa maisha kuongezeka, shenzi airtel!!!!
 
kila nikinunua kifurushi kabla hata sijakitumia wanantumia message kwamba nimetumia 90% of it na huwa nazima data kabla sijajiunga hao call agents ndo kabisa dont bother nilikua na tatizo airtel money i called 100 times skupata msaada mpk nikaenda moroco napo bado walikua wana attitude hao csr wao basi ilimradi tu
 
Ile timiza yao ndio wizi kabisa hiyo riba ni kubwa sana na muda wa kurudisha ni mchache mno
 
nimenunua MB kifuru cha wiki nimedownload app mbili, fb na whatsapp nikashangaa wananiambia kifurushi chako kimeiaha. Imenibidi nihamie.Halotel
 
Nilikua nawaona airtel wajanja kwa hili nabaki nilipo
 
Airtel mnavocha ambazo hazisomi kwenye simu. Nimeenda ofisini mnasema nimtafute aliyeniuzia wakati mi nimenunua kwenye foleni.
 
Hii Airtel TV ndo nini mbona haifanyi kazi hata uwe na bundle??.
Nimenunua kifurushi cha ck mara mbili lakini hata channel moja haijacheza whyyyy!!!.
 
Mimi jana nimewatukana sana, yaani nimejiunga kifurushi cha wiki cha 2000,nikapata sms 300,heee leo asubuhi naambiwa sms zimekwisha!! Nawapigia wananiambia si nimezitumia,, we masaa 5,nimetumia kama sms 5,tu leo unaniambia sms 300,nimezimaliza.
 
Airtel mi niliianzishia uzi hapa.. Pata matatizo yote ila isiwe airtel money...
Ikipokelewa watakwambia "..mtandao wangu unasumbua,kata na upige tena kwa mwenzangu mwingine. Asante kwa kutumia huduma za airtel...!!"
Utaambiwa hivyo na watoa huduma hata 6!!
 
Mimi jana nimewatukana sana, yaani nimejiunga kifurushi cha wiki cha 2000,nikapata sms 300,heee leo asubuhi naambiwa sms zimekwisha!! Nawapigia wananiambia si nimezitumia,, we masaa 5,nimetumia kama sms 5,tu leo unaniambia sms 300,nimezimaliza.

Nami yemenikuta walilamba zote sms 300 na kifurushi cha Internet
 
Back
Top Bottom