May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,367
- 9,110
Kwanza niwapongeze kwa kuwa na huduma hii, ila naomba nitoe ushauri wangu kidogo.
Naomba muwe na utaratibu ambapo kama Mteja ataitumia huduma hii kwa muda mrefu na kwa uaminifu basi walau apate matunda tofauti na wenzake waliokiuka vigezo na masharti.
Kwa mfano kwa nini Mtu aliyetumia huduma hii, kwa miaka mitatu mfululizo kwa uaminifu asiongezewe muda wa kulipa mkopo sambamba na nafuu ya riba? labda sasa awe analipa ndani ya mwezi mmoja na riba ya 10% n.k.
Sitaki kuamini ya kuwa hamfahamu kama huo muda wenu wa kulipa kwa wiki mojia au mbili au tatu( kwa Mteteja kuchagua) na riba zake zile, kwamba zinaumiza sana. Walau basi kuwe na unafuu kadri Mtu napoonyesha uaminifu kwa muda mrefu, badala na hali ilivyo sasa ya nyie kujiangalia tu mnapata nini.
Kwa mtindo huo pia mtaweza kuwavutia Watu wawe waaminifu wakijua faida za kuwa waaminifu ni kubwa kuliko kuleta ujanja ujianja.
Naomba muwe na utaratibu ambapo kama Mteja ataitumia huduma hii kwa muda mrefu na kwa uaminifu basi walau apate matunda tofauti na wenzake waliokiuka vigezo na masharti.
Kwa mfano kwa nini Mtu aliyetumia huduma hii, kwa miaka mitatu mfululizo kwa uaminifu asiongezewe muda wa kulipa mkopo sambamba na nafuu ya riba? labda sasa awe analipa ndani ya mwezi mmoja na riba ya 10% n.k.
Sitaki kuamini ya kuwa hamfahamu kama huo muda wenu wa kulipa kwa wiki mojia au mbili au tatu( kwa Mteteja kuchagua) na riba zake zile, kwamba zinaumiza sana. Walau basi kuwe na unafuu kadri Mtu napoonyesha uaminifu kwa muda mrefu, badala na hali ilivyo sasa ya nyie kujiangalia tu mnapata nini.
Kwa mtindo huo pia mtaweza kuwavutia Watu wawe waaminifu wakijua faida za kuwa waaminifu ni kubwa kuliko kuleta ujanja ujianja.