Airtel Money Acheni Wizi

Airtel Money Acheni Wizi

mashalo

Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
16
Reaction score
3
Nimekuwa mtumiaji mzuri wa Airtel Money kwa muda. sasa tangu walipokuja na slogan yao ya HAKATWI MTU HAPA, nimeshawahi kutumiwa pesa wakailamba hapohapo nilipouliza nikaambiwa tatizo lako linashughulikiwa ndani ya saa 24 itarudi na sasa mwezi unafika mwisho wa siku naambiwa eti hela haionekani, Sio Wizi Huu? Kibaya zaidi hawana Customer Care nzuri kwa wateja kana kwamba mteja kwao ni ---- mbona mitandao mingine kama VODACOM wako active, wakikuambia tunashughulikia tatizo lako ndani ya muda walioahidi wanatimiza ahadi? Airtel Money mna NINI? ACHENI WIZI
 
Ndugu yangu ogopa sana mtu anayetoa huduma bure. Unafikiri atapataje faida. Ni lazima akatwe mtu kama ulivyokatwa wewe ili faida ipatikane.
 
Tatizo ni letu wenyewe serikali walishaweka tozo la hizi pesa zinapotumwa iwe kupitia simu au benki sasa hiyo kodi jiulize nani anailipa kwa serikali kama sio wewe mtumiaji? Amkeni msidanganywe kodi lazima ilipwe kwa tra
 
Mi nilinunua kifurushi cha wiki cha shs 9999 lakini nilipompigia mtu nikaongea 1dk kifurushi kwisha,nikapiga customer care nikasubirishwa saa zima na kitu lakini walipopokea nikaambiwa ni tatizo system hivo watalishughulikia na baada ya masaa matatu litakuwa solved,masaa yakasonga hatimae siku mbili nikapiga tena majibu ni yale yale wakanambia ndani ya saa moja litakuwa solved, siku mbili nkapiga tena mambo yale yale hatimae wiki imeisha bila kifurushi.

Nimeamua kubadili mtandao nione wizi mwingine wa voda japo ukiwa na tatizo wanalisolve kwa mda mfupi bila longo longo.
 
Mimi tangu nianze kutumia hii huduma sijawahi kuona tatizo.
 
Mitandao ya simu karibu yote ni wezi.

Ukitaka kujua jaribu kuwa una-monitor salio lako kwenye simu kila wakati.

Amini nawaambieni lazima utagundua kuna kiwango kinakatwa walau kila siku. Walivyo wajanja huwa hawakati hela nyingi, ni kiwango kidogo sana ambacho huwezi kugundua kama hufuatilii. Pia wanajua kabisa kuwa mtu atadharau hata akigundua kuwa amekatwa.

Wanaweza kukukata kati ya shilingi moja hadi 30 hivi. Ukiwauliza wanakujibu kwa nyodo huenda ulijiunga na huduma fulani halafu wanakata simu.

Cha kusikitisha mamlaka ya kusimamia mawasiliano haiko kwa ajili ya wateja bali watoa huduma.
 
Back
Top Bottom