Airtel mmeamua kutusaliti?

Airtel mmeamua kutusaliti?

nilianza na vodacom wakaniboa nikahamia tigo wakaniboa nikarudi vodacom tena wakaja kuniboa nikahimia airtel sasa tena naona wanataka kuniboa tena na wao ntarudi nilikotoka sijajuwannini kimewakuta labda ghalama za umeme sijuwi
 
Yaani wameniboa kuliko maelezo nilikwa nanunua kifurushi 19999 napata dk 650 nimeshangaa leo napata dk450 wiZi mtupu tuhamie mtandao gani zantel vp?

Wanayo epiq sh 800 dakika 40, mb 500 day.

Sent from my GT-I9192 using Tapatalk
 
Umeona eh! Voda walikua na ujinga huohuo.ila nawapongeza kwa kusikiliza maoni ya wateja wao!
 
Nimekuwa mtumiaji mzuri wa vifurushi vya airtel na nimewashawishi ndugu rafiki wengi kuhamia mtandao huu kutokana na huduma nzuri ila leo nimeumia sana naamka asubuhi kujiunga na na kifurushi cha sh 5999 ambacho ni wiki nzima yenye dakika 200 sms nyingi tu sikumbuki kwakuwa si mpenzi wa sms, 2gb za internet ndicho kivutio kabisa.
Nimeshangaa eti wamebadiri tena bila taarifa dakika 135 , sms 1000 hazina maana kibaya zaidi net ni 500mb! hivi kweli mmeaza tabia za washindani wenu ambao nao baada ya kuanza kupoteza wateja wamejirekebisha!
Nawaambia kama niliwajenga hata kuwabomoa naweza, kuna mtandao mpaka leo wananiomba walau niweke mia nimegoma na line iko hewani tu
Mjirekebishe la sivyo tutaharibiana kaeni mfikirie upya efu sita ni pesa nyingi sana acheni utani.
Hakuna kitu hapo
 
Wanajiona wamepata kumbe sisi ndo wawezeshaji,mi ni metupa line ya vod,tigo nikaingia airttell nikidhan wako makini kumbe nao ni washenzi wa tabia
 
Hata mimi nimeshindwa kuwaelewa na pia wasisingizie kupanda kwa umeme n.k. Kama kupanda kwa gharama za uendeshaji siyo kwa airtel tuu na kwa watoaji huduma wengine.

Walivyoanzisha hizo huduma za siku, wiki, mwezi n.k walitutangazia na ndio maana tukajiunga nao. Sasa wanavyopandisha bila kutoa taarifa wana maanisha nini?
Mimi tokea nilivyogundua juzi nimeanza kuwakimbia, na wasipojirekebisha najua wateja wengine watawakimbia.....
 
Kumbe?!nimeona kuanzia jana yaani wameondoa lile bando la 2999.
 
Back
Top Bottom