nessonlegend
JF-Expert Member
- Mar 1, 2013
- 1,698
- 1,507
Mnamo tarehe 16-1-2019 nimekopa salio kupitia huduma ya airtel inayopatikana kupitia menyu *149*99# >1 ofa maalumu >3 kopa bando >4 kopa salio. katika kipengele cha namba 3 hapo kuna option za kuchagua mfano unataka kukopa muda wa hewani toka airtel kwenda airtel, au kwenda mitandao yote, au unataka kukopa kifurushi cha intaneti, pia kuna hiyo namba 4 ambayo ukiichagua ndiyo kuna option ya kiasi cha muda wa maongezi unaotaka kupatiwa.
Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba pamoja na kuchagua muda wa hewani, wanakuletea ujumbe kuwa umepokea kiasi fulani toka huduma ya DAKA, na wakati huo huo ukiangalia salio kupitia *102# wanakuletea ujumbe kuwa hauna salio ila una deni la kiasi fulani likiwa limeongezwa na tozo kama riba ya mkopo.
Baada ya kutafakari nikapiga namba 102 ili kuangalia salio kwa njia ya sauti ndiyo wanaleta ujumbe kuwa una dakika kadhaa na deni la shilingi kadhaa. Nilikasirika sana tena sio kidogo (nilitumia hii huduma kwasababu ilikuwa usiku na nilikuwa nahitaji salio niunge night park ya GB). nikajikuta najiuliza maswali haya yafuatayo:
a) Ni kwanini wananipangia matumizi ilihali pesa wamenikopea na wanahitaji kulipwa na riba?
b) Wana uhakika gani kuwa nilikuwa nahitaji dakika za kuwasiliana na watu na wakati nimekopa muda wa maongezi?
c) Mbona kuna option yakukopa vifurushi na muda wa hewani tofauti afu mtu ukikopa muda wa hewani unapatiwa dakika bila ya maelezo yoyote?
d) Je, huu sio wizi tuaofanyiwa na huu mtandao?
e) TCRA wanajua hii dhuruma tunayofanyiwa watu tunaotomia mtandao huu?
Leo tarehe 17-1-2019 asubuhi nimelipa deni lao lakini hawaleti hata taarifa kuwa umefanikiwa kurejesha deni lako kama ilivyo katika mitandao mingine, hata dakika zao wanazoziseha sijazitumia kwani sikuwa nashida nazo. HUU WIZI TUSIFUMBIE MACHO WADAU WA JF.
Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba pamoja na kuchagua muda wa hewani, wanakuletea ujumbe kuwa umepokea kiasi fulani toka huduma ya DAKA, na wakati huo huo ukiangalia salio kupitia *102# wanakuletea ujumbe kuwa hauna salio ila una deni la kiasi fulani likiwa limeongezwa na tozo kama riba ya mkopo.
Baada ya kutafakari nikapiga namba 102 ili kuangalia salio kwa njia ya sauti ndiyo wanaleta ujumbe kuwa una dakika kadhaa na deni la shilingi kadhaa. Nilikasirika sana tena sio kidogo (nilitumia hii huduma kwasababu ilikuwa usiku na nilikuwa nahitaji salio niunge night park ya GB). nikajikuta najiuliza maswali haya yafuatayo:
a) Ni kwanini wananipangia matumizi ilihali pesa wamenikopea na wanahitaji kulipwa na riba?
b) Wana uhakika gani kuwa nilikuwa nahitaji dakika za kuwasiliana na watu na wakati nimekopa muda wa maongezi?
c) Mbona kuna option yakukopa vifurushi na muda wa hewani tofauti afu mtu ukikopa muda wa hewani unapatiwa dakika bila ya maelezo yoyote?
d) Je, huu sio wizi tuaofanyiwa na huu mtandao?
e) TCRA wanajua hii dhuruma tunayofanyiwa watu tunaotomia mtandao huu?
Leo tarehe 17-1-2019 asubuhi nimelipa deni lao lakini hawaleti hata taarifa kuwa umefanikiwa kurejesha deni lako kama ilivyo katika mitandao mingine, hata dakika zao wanazoziseha sijazitumia kwani sikuwa nashida nazo. HUU WIZI TUSIFUMBIE MACHO WADAU WA JF.