Ndugu zangu nilijiunganisha na airtel 5g unlimited internet nikajua kwamba hawana limit ya volume kumbe unahesabiwa gb na GB zikiisha speed ya internet inapungua. Mimi nilitoka kuwa na speed ya download 30Mbps Upload 5OMbps kwenda mpaka 1Mbps download na 2Mbps upload daah nichangamoto kubwa sana.
Nawashauri tu wale ndugu zangu wanaotaka kujiunga na hii airtel 5g unlimited. Kama wewe ni mtu wa kudownload vitu sana hii haifai kabisa na speed ikipungua internet inasumbua yani hata kuchek tu insta shughuli ina stuck sana.
Unlimited ya kweli labda kama fiber inafika kwako ila hizi za minara ya simu ngumu maana wengi mnakua mna share bandwidth ya mnara na mkiwa wengi ni majanga kwao
Unlimited ya kweli labda kama fiber inafika kwako ila hizi za minara ya simu ngumu maana wengi mnakua mna share bandwidth ya mnara na mkiwa wengi ni majanga kwao
Users kwenye hio bandwidth uliyopewa au wateja wote wa hilo eneo?? Kwa airtel sijajua kwenye 5G sasa ila chini ya hapo ilikua lazima ikifika kiwango fulani wanapunguza speed