Aingiza Bilion 7 ndani ya siku mbili

Aingiza Bilion 7 ndani ya siku mbili

Mstahiki Mea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
5,581
Reaction score
10,110
1773555529317.jpeg


Jinsi Rostam Aziz Alivyoingiza Zaidi ya TSh Bilioni 7 Ndani ya Siku Mbili Kupitia Hisa Bila Kuuza chochote

Kama humjui Rostam Aziz, ni mmoja wa wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji wenye ushawishi Afrika Mashariki.

Amewekeza katika sekta nyingi kama nishati, mawasiliano na viwanda.

hiyo Siyo mada ya Leo...

wiki hii kulikuwa na jambo la kuvutia zaidi.

Rostam Aziz Kupitia kampuni yake Taarifa Ltd, Rostam Aziz alitangaza kununua 54.08% ya hisa za Nation Media Group (NMG) ya Kenya.

NMG ni moja ya makampuni makubwa ya media Afrika Mashariki inayomiliki vyombo kama:

Daily Nation

NTV Kenya

The East African

Na Tanzania wanamiliki magazeti kama:

Mwananchi

The Citizen

Mwanaspoti

Baada ya tangazo hilo…

Bei ya hisa za NMG ilipanda kwa zaidi ya 28.3% ndani ya siku mbili tu.

Kabla ya tangazo:

Hisa zilikuwa KSh 13.25

Baada ya tangazo:

Zilipanda hadi KSh 17 kwa hisa

Kwa kuwa NMG ina zaidi ya hisa milioni 190, na Rostam anamiliki zaidi ya 50%.

kupanda huko kwa bei ya hisa kuliongeza thamani ya uwekezaji wake kwa makadirio ya zaidi ya TSh bilioni 7 ndani ya siku mbili.

Na hapa ndipo siri ya uwekezaji ilipo.

Rostam hakuchapisha magazeti.

Hakuuza habari.

Hakutangaza matangazo.

Alinunua hisa.

Na thamani ya uwekezaji wake ikaongezeka kutokana na kupanda kwa bei ya hisa.

Ndiyo maana utajiri mkubwa duniani haujengwi kwa kufanya kazi tu…

Unajengwa kwa kumiliki assets kama:

Hisa za makampuni

Biashara

Uwekezaji

Kwa sababu kampuni inapokua, thamani ya hisa inapanda na wewe kama mwanahisa utajiri wako unaongezeka.

Hapa Tanzania pia kuna Dar es Salaam Stock Exchange (DSE) ambapo unaweza kununua hisa za makampuni kama:

CRDB

NMB

TBL

TCC

Vodacom

Credit: Kutoka kwa Mdau
 
Back
Top Bottom