Aina za ndoa 2023

jay-millions

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2015
Posts
4,475
Reaction score
11,474
1. NDOA YA MKEKA
Inatokana na kufumaniwa na Binti wa watu. Ndoa hii huwa Haina mahari. Hii huvunjika mwaka mmoja tu baada ya wanandoa kugundua hawakuwa wakipendana!

2. NDOA YA MIHEMKO (NYEGE)
Hufungwa na vijana wenye umri wa miaka kati mume18 mke 16. Huvunjika baada ya miaka 3 au 4 ya ndoa.

4. NDOA YA MAONYESHO
Wenye ndoa Hii hupenda kujionyesha barabarani. Ila ndani hazina utii. Hupigana kila wanaporudi kutoka kwenye mizunguko. Cha kushangaza huwa hazivunjiki lakini ndiyo ndoa zinazoongoza kwa kuchepuka!

5. NDOA YA UHAMISHO.
Hufungwa na watumishi wa vijijini na mjini. Ili wa kijijini ahamie mjini. Mahari hutoa anayetaka kuhamia mjini. Hata kama mahari atatoa mume lakini hii ndiyo ndoa yenye ukakasi zaidi.Huvunjika mara tu wanapoanza kuishi wote mjini. Salama ya hii ndoa ni kuhama kutoka mjini kwenda kijijini.

6. NDOA YA MIMBA.
Hufungwa kwa sababu wanaoowana hawataki kuonekana makwao kuwa wamezaa nje. Au muolewaji alikuwa hampendi muoaji kwa dhati.Muoaji hutumia mimba kama mtego wa kuingia ndoani. Hii huvunjika mtoto akizaliwa na kufikisha mwaka 1.

7. NDOA YA MALI (UTAJIRI)
Muolewaji miaka 18 au 28 Muoaji 65 au 70.Ndoa hii pia huitwa ndoa ya babu na mjuukuu. Ndoa ya aina hii hudumu, kwasababu mwenye kauli ni mwenye mali. Asilimia kubwa ya waume wa ndoa hizi hulea watoto wasio wao.

8. NDOA YA KWA SABABU.
Hufungwa ili mradi muoaji au muolewaji aonekane tu kwa jamii kuwa naye kaoa au kaolewa. Huwa hazina utii wala upendo dhati. Ndoa ya aina hii ikifikisha miaka 4 huwa hazivunjiki wahusika huishi kwa mazoea.

9. NDOA YA UPENDO.
Ndoa hizi ziliishia mwaka 1978 kabla ya vita vya Kagera. Muoaji na muolewaji hawakuangalia vitu ila utu tu ambao uliwaunganisha na kutengeneza upendo wa kudumu. Hii ilidumu miaka yote.

10. NDOA KUCHUMA
Ndoa hii ufungwa ili mradi muoaji au muolewaji akapate kitu au vitu fulani kutoka kwa upande mmoja wapo. Hii hudumu miaka kadhaa kutegemea na malengo ya mhusika. Wengine husubiri mpaka mhusika afe,lkn hujikuta wanakufa wao kwanza

11. NDOA ZA HUDUMA
Hii hufungwa baada ya binti au kijana kuona anaweza jipatia matunzo kiulaini kama kula bure, kulala kuvishwa, kupewa gari na vingine kama hivyo kutoka kwa mwenza, hudumu sana mpaka pale mtunzaji atakapo shindwa au kuchoka kumhudumia mhusika hapo ndo mhudumiwaji atahamia kwingine. Hizi ndo nyingi kwa sasa na ndo zinaongoza kutrend instagram.

12. NDOA ZA KUSOGEZANA
Hizi vijana ambao hawajajipanga huamua kuanza kuishi pamoja huku wakikusanya mahari na hela ya harusi, hizi changamoto yake ni jambo la kufunga ndoa ambalo lingeweza kufanyika ndani ya mwaka basi laweza fanyika baada ya miaka kumi. Hizi pia hudumu sana na binti huzaa chap chap ili kujimilikisha nafasi asije achwa
 
Za mimba ndo zipo kibao kwa sasa ndo zinawatesa watu nimeshuhudia sana.
 
Hiyo namba 5 kuna demu nayedate naye anaimendea ila mjuba mapema nishamshtukia 🀣🀣🀣
 
Hiyo #2 hata walio kwenye 30’s-40’s wanafunga, mwisho wanaingia cha kike
 
ukiwa mwanaume na ndoa yako ni aina ya namba 5, ikiwa mna watoto si ajabu wengine si wako. Ni ndoa zinazoongoza wanandoa kuchepuka. Na wanandoa wengi katika ndoa hii huwa hawalali chumba kimoja. Kila mmoja anajua anavyoingia na kutoka. sterling wa nyumba ni housemaid
 
Ha ha ha.....
Hiyo namba moja sio Kweli,
Mi nmeshuhudia zikidumu sana
Hio namba moja huwa ni kama ndoa ya nyege tu sema wazazi wa upande mmoja wanakomalia uoe kabisa au binti aolewe kabisa. Kama kweli mlipendana mnadumu ila kibaya ni kwamba huwa zinawatokea sana mabinti wakiwa katika enzi za usichana mbichi.

Anapokuwa akili inabadilika vipaumbele vinabadilika anajikuta aliemuoa sio mwanaume ambaye angependa kufanya nae maisha.

Hio kuna pisi moja tulipiga nayo degree. Yule demu alikuwa ni mzuri sana ana haiba ya upole na adabu zake. Sofia mtoto wa kiislamu yani ukimuona ni pure wife material. Ila akiwa form 5 alitiwa mimba na mwalimu mmoja baada ya kuua 6 akaolewa cha mkeka.

Kaja first year ana stress za ndoa balaa mumewe ana mawivu basi mda wote sofia mtu wa mawazo na she was very bright on top of all the girls darasani alikuwa ana lead kwa high scores. Saingine anapigwa huko akija ana uchungu balaa wa ndoa.

Imagine msichana mdogo tu second year ndio akili inafunguka anaona wenzie wanavyodate na agemates jinsi ilivyo raha. Wanavyokuwa treated kwa raha. Yule demu mambo yakazidi kuwa ndivyo sivyo baada ya mwaka wa tatu nafikiri alipewa talaka yake akamove on.

Haikuchukua mwaka akaolewa na mtu wa kueleweka sana Dodoma. Anakula zake apple tu sahizi na watoto na familia mpya.
 
Kidogo hizi ndo zimepungua mjini.
 
Of all ndoa namba #10 ndio ndoa inayoongoza kwa kufungwa na vijana na maslay queen wa mjini.

Haidumugi sababu msingi wa ndoa ni huduma. Mwanaume anakuwa ameielewa shape na muonekano wa demu ila demu anakuwa amependa lifestyle ya mwanaume huyo. Pesa ya kula bata na magari ya kufanyia starehe za town.

Ikitokea tu mwanaume hela zimekata ndio mgogoro unapoanzia tena vijembe na kejeli za mwanamke hutajua zilipotokea. πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€ Kumbe alikuwa anakudanga tu kabla hujatumbuliwa.
 
Ni ndoa ambazo zimejaa usanii na maigizo

Kislay queen kitakuugizia kinakupenda kinyama kitakupost sana kwenye mitandao mkiwa maeneo mazuri au mkiwa mnakula bata

Ukifilisika vijembe vinaanza hawachelewi kufuta post zake zote enzi hizo mkiwa mnakula bata mpunga ulipokuwepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…