Aina za marafiki katika maisha yetu

Apr 18, 2012
95
213
18118917_746509435530637_4690404843500178251_n.jpg

1f449_1f3fb.png
Kuna mengi hatujui kuhusu marafiki zetu.
Kuna watu wameumizwa na marafiki zao kwa sababu hawakuwa na macho ya rohoni kuweza kuwatazama.
Kama wewe ni mmoja kati ya wale ambao marafiki wamekuwa jaribu, basi somo hili na likawe msaada kwako.

31_20e3.png
1⃣ *CONFIDANTS*
Hili ni kundi la kwanza la marafiki.
“Confidants” ni wale marafiki wanaokupenda bila masharti. Wako nawe ukiwa juu au chini, ukiwa tajiri au maskini, ukiwa sahihi au ukikosea, wako pamoja na wewe. Ukipelekwa gerezani watakufuata, ukilia watalia pamoja nawe, na ukifurahi watafurahi pamoja nawe. Ni watu ambao unakuwa huru zaidi kuwaeleza kila jambo kuhusu maisha yako (kuliko hata ndugu zako) na kwa kufanya hivyo unajikuta unafarijika na kupata amani moyoni. Hutaweza kutimiza maono yako bila kuwapata “Confidants” wako.
1f449_1f3fc.png
Confidants ndio wanaoelezwa katika Mithali 18:24; kuwa ni marafiki wanaoambatana na mtu kuliko ndugu. Mungu anakuletea watu kama hawa kwenye biashara, katika huduma, katika uongozi n.k. ili wakusaidie kwa maombi, ushauri na kukuonya, ili uweze kufanikiwa kama Mungu alivyokusudia. Ukipata wawili au watatu katika maisha yako, basi wewe ni mtu uliyebarikiwa sana, kwa sababu bila watu hawa hutaweza kuwa vile Mungu alivyotaka uwe. Usiwapoteze confidants wako kirahisi. Mungu akusaidie uwe confidant kwa mtu fulani.

32_20e3.png
2⃣ *CONSTITUENTS*
Hawa ni marafiki hatari, kwa sababu hawako kwa ajili yako, wapo kuiba maono yako. Ni wezi wa maono. Biblia inasema pasipo maono watu huangamia (Mithali 29:18); Kwa hiyo anayekuibia maono kwa lugha nyingine amekuangamiza. Unakuta binti amepata mchumba, (au hata wakaka sometimes!!!!) anamshirikisha rafiki yake kile Bwana alichomtendea, lakini baada ya muda mfupi anaachwa na anashangaa rafiki yake mtu aliyemuamini saaaaaana amemuibia mchumba. Watu wengi wameumizwa na marafiki kwa namna hii but kiukweli hawasemi tu.. Huyo alikuwa rafiki aina ya “constituent”, unachotaka ndicho anachotaka. Ole wako wewe mwenye constituent kwenye mahusiano au biashara yako ukidhani ni confidant. Ukimueleza constituent habari za mchumba wako atakuibia (abiria chunga mzigo wako!!!) Ukimueleza constituent habari za wazo la biashara unayotaka kuanzisha atakuibia hilo wazo.
1f449_1f3fb.png
Kumbuka vizuri habari za Yakobo na Esau, Yakobo alikuwa “constituent” kwa Esau, akamwibia baraka. Na Mungu amekupa marafiki kama hawa kwa lengo moja kubwa, _kukufundisha kwa vitendo kwamba maono yako yanaweza kuibiwa usipoyalinda_ .. Mungu akupe “MACHO” ya kuwajua constituents katika maisha yako.

33_20e3.png
3⃣ *COMRADES*
Hawa ni marafiki ambao Mungu anawaleta katika maisha yako kwa kusudi maalumu, sometimes kwa muda maalumu tu na baada ya hapo hutawaona tena. Ni watu wanaopigana na kile unachopigana nacho, kukusaidia kushinda upinzani mkubwa na baada ya hapo hutawaona tena. Sasa usipate shida wakikuacha na kuondoka, hawa hawatadumu nawe kipindi kirefu. Hawa ni kama ngazi (ladder) ambayo inahitajika sana wakati nyumba inajengwa, lakini nyumba ikishakamilika ngazi itaondolewa ila nyumba itabaki.

1f449_1f3fb.png
Simoni mkirene alionekana tu wakat wa kumsaidia Yesu msalaba na kuufikisha Golgotha, baada ya hapo hatujui alielekea wapi (Mt 27:32). Pia kumbuka Yonathani alivyomsaidia Daudi kupigania nafasi yake ya ufalme, na baadaye tunaambiwa Yonathani mwenyewe akafa muda mchache kabla hata Daudi hajalipa fadhila (2 Sam 1:26), kwa sababu Yonathani alikuwa Comrade wa Daudi. Huwezi kuwa Daudi bila kumpata Yonathani wako!! Pia kumbuka namna Filipo alipomsaidia Towashi wa Kushi kuokoka. Baada tu ya kumbatiza, Biblia inasema Filipo akachukuliwa na Roho mtakatifu. Comrades si marafiki wa kudumu.

❇NB.
Wako marafiki wengine hawako kwenye kundi lolote kati ya hayo niliyoyataja hapo juu.
Hao nawaita “wrong partners”. Hutaweza kufika unakokwenda usipojitenga nao mapema. Mkumbuke Yona. Watu wote kwenye meli wangeangamia kama wasingemtupa Yona baharini. He was a wrong partner (japo ni mtumishi wa Mungu). Mtupe Yona wako, ili ufike salama. Kuna huduma zimekwama, kuna makampuni yamerudi nyuma, kuna biashara zimefilisika kwa sababu wamembeba Yona bila kujua atawaletea shida safarini.. mtupe
Yona wako, Tafuta Confidants wako,..
 
Tatizo Uzi umeekuwa wa kidini sana japo kuna mantiki
Sisi tusioamini maandiko ya dini umekuwa kikwazo kuamini hii nyuzi
 
Asante mkuu...
Ili uwe na mafanikio maishani hauhitaji marafiki zaidiya watano!
 
*USIYOYAJUA KUHUSU MARAFIKI* -

Kuna mengi hatujui kuhusu marafiki zetu.
Kuna watu wameumizwa na marafiki zao kwa sababu hawakuwa na macho ya rohoni kuweza kuwatazama.
Kama wewe ni mmoja kati ya wale ambao marafiki wamekuwa jaribu, basi somo hili na likawe msaada kwako.

1⃣ *CONFIDANTS*
Hili ni kundi la kwanza la marafiki.
“Confidants” ni wale marafiki wanaokupenda bila masharti. Wako nawe ukiwa juu au chini, ukiwa tajiri au maskini, ukiwa sahihi au ukikosea, wako pamoja na wewe. Ukipelekwa gerezani watakufuata, ukilia watalia pamoja nawe, na ukifurahi watafurahi pamoja nawe. Ni watu ambao unakuwa huru zaidi kuwaeleza kila jambo kuhusu maisha yako (kuliko hata ndugu zako) na kwa kufanya hivyo unajikuta unafarijika na kupata amani moyoni. Hutaweza kutimiza maono yako bila kuwapata “Confidants” wako.
Confidants ndio wanaoelezwa katika Mithali 18:24; kuwa ni marafiki wanaoambatana na mtu kuliko ndugu. Mungu anakuletea watu kama hawa kwenye biashara, katika huduma, katika uongozi n.k. ili wakusaidie kwa maombi, ushauri na kukuonya, ili uweze kufanikiwa kama Mungu alivyokusudia. Ukipata wawili au watatu katika maisha yako, basi wewe ni mtu uliyebarikiwa sana, kwa sababu bila watu hawa hutaweza kuwa vile Mungu alivyotaka uwe. Usiwapoteze confidants wako kirahisi. Mungu akusaidie uwe confidant kwa mtu fulani.

2⃣ *CONSTITUENTS*
Hawa ni marafiki hatari, kwa sababu hawako kwa ajili yako, wapo kuiba maono yako. Ni wezi wa maono. Biblia inasema pasipo maono watu huangamia (Mithali 29:18); Kwa hiyo anayekuibia maono kwa lugha nyingine amekuangamiza. Unakuta binti amepata mchumba, (au hata wakaka sometimes!!!!) anamshirikisha rafiki yake kile Bwana alichomtendea, lakini baada ya muda mfupi anaachwa na anashangaa rafiki yake mtu aliyemuamini saaaaaana amemuibia mchumba. Watu wengi wameumizwa na marafiki kwa namna hii but kiukweli hawasemi tu.. Huyo alikuwa rafiki aina ya “constituent”, unachotaka ndicho anachotaka. Ole wako wewe mwenye constituent kwenye mahusiano au biashara yako ukidhani ni confidant. Ukimueleza constituent habari za mchumba wako atakuibia (abiria chunga mzigo wako!!!) Ukimueleza constituent habari za wazo la biashara unayotaka kuanzisha atakuibia hilo wazo.
Kumbuka vizuri habari za Yakobo na Esau, Yakobo alikuwa “constituent” kwa Esau, akamwibia baraka. Na Mungu amekupa marafiki kama hawa kwa lengo moja kubwa, _kukufundisha kwa vitendo kwamba maono yako yanaweza kuibiwa usipoyalinda_ .. Mungu akupe “MACHO” ya kuwajua constituents katika maisha yako.

3⃣ *COMRADES*
Hawa ni marafiki ambao Mungu anawaleta katika maisha yako kwa kusudi maalumu, sometimes kwa muda maalumu tu na baada ya hapo hutawaona tena. Ni watu wanaopigana na kile unachopigana nacho, kukusaidia kushinda upinzani mkubwa na baada ya hapo hutawaona tena. Sasa usipate shida wakikuacha na kuondoka, hawa hawatadumu nawe kipindi kirefu. Hawa ni kama ngazi (ladder) ambayo inahitajika sana wakati nyumba inajengwa, lakini nyumba ikishakamilika ngazi itaondolewa ila nyumba itabaki.

Simoni mkirene alionekana tu wakat wa kumsaidia Yesu msalaba na kuufikisha Golgotha, baada ya hapo hatujui alielekea wapi (Mt 27:32). Pia kumbuka Yonathani alivyomsaidia Daudi kupigania nafasi yake ya ufalme, na baadaye tunaambiwa Yonathani mwenyewe akafa muda mchache kabla hata Daudi hajalipa fadhila (2 Sam 1:26), kwa sababu Yonathani alikuwa Comrade wa Daudi. Huwezi kuwa Daudi bila kumpata Yonathani wako!! Pia kumbuka namna Filipo alipomsaidia Towashi wa Kushi kuokoka. Baada tu ya kumbatiza, Biblia inasema Filipo akachukuliwa na Roho mtakatifu. Comrades si marafiki wa kudumu.

❇NB.
Wako marafiki wengine hawako kwenye kundi lolote kati ya hayo niliyoyataja hapo juu.
Hao nawaita “wrong partners”. Hutaweza kufika unakokwenda usipojitenga nao mapema. Mkumbuke Yona. Watu wote kwenye meli wangeangamia kama wasingemtupa Yona baharini. He was a wrong partner (japo ni mtumishi wa Mungu). Mtupe Yona wako, ili ufike salama. Kuna huduma zimekwama, kuna makampuni yamerudi nyuma, kuna biashara zimefilisika kwa sababu wamembeba Yona bila kujua atawaletea shida safarini.. mtupe
Yona wako, Tafuta Confidants wako,..
Much love
asante sana baba mchungaji .ila soma biblia yako vizuri daudi alikuja kumlipa yonathan fadhila kubwa sana .
 
Back
Top Bottom