Habari wadau,
Leo nilikimbia kidogo ukweni kusalimia wazee wangu walionizalia mke wangu mzuri.. Baada ya kupiga story na kupata msosi tukaanza kufunga mizigo (ya kumletea mtoto wao nyumbani) wakata kuku wawili jogoo na jike wanakimbizana, bahata nzur kufika pale jike akakosa njia na jogoo likaanza kazi.
Aibu imekuja hapa, ni nani asimame amfukuze awafukuze? Mimi nikavunga na baba mkwe kavunga, mama mkwe kasimama kwenda kuwafukuza ila anapiga hatua akatereza akaanguka... mimi nilikosa cha kusema na baba mkwe akakosa cha kusema yaan tukakaa tumetazamana tu.
Mila zetu haziruhusu kijana kumgusa mama mkwe ningeenda kusaidia, ashukuriwe Mungu baba alikuwepo.