Ahadi Kuu ya Kikwete (Kigezo cha Uwezo/Udhaifu wake)

MgungaMiba

JF-Expert Member
Aug 28, 2011
999
815
Ada ya mja hunena " Uungwana ni Kitendo" na Vitabu vya dini vinasema kuwa moja ya Dalili za Mnafiki ni Atoapo Atoapo Ahadi Hatekelezi. Mwaka 2005 wakati Kikwete akiwania Urais, "Ahadi Yake Kuu ilikuwa "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania Ndani ya Miaka 5" Sasa muda huo tayari umepita na mingine inayoyoma kwa hiyo si vibaya kufanya Stock Taking na kumtathmini huyu mtu. Je hivi sasa kila Mtanzania ana Maisha Bora! Au Bora Maisha? Kama hajatekeleza ahadi hii basi atakuwa Nia alikuwa nayo bali UDHAIFU wake ndio uliomfanya ashindwe kutekeleza Ahadi yake au Ni Mnafiki kwani ameahidi jambo analojua halitekelezeki. Yuko kwenye Position ya Catch 22 (yuko kwenye Chombo kinachozama, Kuogelea Hajui na Majini kuna Papa wala watu wenye njaa!) Kwa hiyo ni DHAIFU au MNAFIKI, sijui ni lipi lenye afadhali.
 
Back
Top Bottom