MkenyaMzalendo
Senior Member
- Sep 12, 2010
- 171
- 16
Naona sasa mnanichekesha! Paypal ni njia mojawapo tu ya kutuma na kupokea pesa wala sio indication ya nguvu za kiuchumi wa nchi husika. Kumbukeni kuwa hata kwa nchi ya Afrika Kusini huduma za Paypal zimeanza mwanzoni mwa mwaka huu na ni kwa kupitia benki moja tu ya FNB kwa hiyo kama unataka kutuma ama kupokea pesa kwa njia hii ni lazima uwe na akaunti ya FNB.
Ni mda mrefu tu wafanyabiashara za mtandaoni wamekuwa wakitaka hii huduma lakini sheria kali za nchi katika udhibiti wa mzunguko wa pesa especially kutuma pesa nje ya Afrika Kusini ndio zilikuwa kikwazo na wala sio issue kwamba Afrika Kusini ina uchumi mbovu!!.
Kumbukeni kuna huduma nyinginezo za kutuma pesa mtandaoni amabazo zinapatikana karibia nchi zote duniani na ni simple zaidi ya Paypal (Paypal wanataka lazima uwe na credit card kwa mtumiaji wa nchi nyinginezo ukiondoa US). Mfano mmoja ni huduma iitwayo Moneybookers ambapo mtumaji na mpokeaji wanatakiwa wawe na e-Mail address tu.
Hii dhana ya ukubwa wa uchumi na huduma za kutuma pesa za Paypal ni potofu!!!:focus:
Ningekualika kutazama nchi zote husika katika huu mfumo wa PayPal katika tovuti www.paypal.com/worldwide . Nakuhakikishia hutopata nchi ambayo uchumi wake ni mdhaifu. Lakini sitaki hio iwe hoja. Natumai utakubaliana nami PayPal hishirikisha nchi ambazo zimeweka mikakati shwari kupigana na ulanguzi wa fedha, nchi ambazo benki zao ni imara kabisa, na pia, nchi ambazo raia wake sio watu wanaopenda kuvuna chenye hawakupanda, thibitisho kamili shutuma (sana sana kutoka kwa WaTz) eti wakenya ni watu walaghai hazina msingi wowote. na labda hili ndilo limefanya PayPal kukwepa nchi kama vile Nigeria, Russia na Ukraine.