Afrobarometer: Janga la ustawi wa taifa letu

Afrobarometer: Janga la ustawi wa taifa letu

mbeyaman

Member
Joined
Sep 28, 2013
Posts
97
Reaction score
28
Taasisi kama Afrobarometer ni kikwazo kikubwa katika mustakabali wa taifa letu.Utafiti uchwara wa taasisi hii umekosa mashiko na tija kwa Watanzania.

Sidhani ni kweli kwamba mh.Rais Jakaya Kikwete anapendwa na watu wasio kuwa na elimu,na hata kama wakimpenda na kukubali utendaji wake wa kazi kuna tatizo gani?

Kwani Watanzania kwa sababu mbalimbali waliokosa elimu hata kama wanampenda rais JK ni utashi wao,taasisi uchwara ya Afrobarometer wanataka hiyo jamii ya waliokosa elimu wampende nani?wampende rais Kagame wa Rwanda?

Mh.Rais anapendwa na Watanzania wote,wasomi na wasio wasomi.

Sera nzuri za CCM na uwezo mkubwa wa uongozi wa mh.JK vimepelekea Watz wampe ridhaa ya kuongoza taifa letu.Katika kipindi cha uongozi wa JK Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo.

Maendeleo ya sasa hivi yameyapita nchi mbalimbali za Afrika.Hivyo taasisi kama Afrobarometer zinatakiwa ziogopwa kama ukoma kwani zinamalengo mabaya ya kuchonganisha wananchi na serikali yao.

Nina mashaka taasisi kama hizi zinatumiwa na baadhi ya vyama vya upinzani ili kuondoa mshikamano na umoja wa kitaifa kwa Watanzania hivyo kuleta vurugu.
 
Na mtakoma mwaka huu...mwendo mchibuyu
 
Taasisi kama Afrobarometer ni kikwazo kikubwa katika mustakabali wa taifa letu.Utafiti uchwara wa taasisi hii umekosa mashiko na tija kwa Watanzania.Sidhani ni kweli kwamba mh.Rais Jakaya Kikwete anapendwa na watu wasio kuwa na elimu,na hata kama wakimpenda na kukubali utendaji wake wa kazi kuna tatizo gani?Kwani Watanzania kwa sababu mbalimbali waliokosa elimu hata kama wanampenda rais JK ni utashi wao,taasisi uchwara ya Afrobarometer wanataka hiyo jamii ya waliokosa elimu wampende nani?wampende rais Kagame wa Rwanda?Mh.Rais anapendwa na Watanzania wote,wasomi na wasio wasomi.Sera nzuri za CCM na uwezo mkubwa wa uongozi wa mh.JK vimepelekea Watz wampe ridhaa ya kuongoza taifa letu.Katika kipindi cha uongozi wa JK Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo.Maendeleo ya sasa hivi yameyapita nchi mbalimbali za Afrika.Hivyo taasisi kama Afrobarometer zinatakiwa ziogopwa kama ukoma kwani zinamalengo mabaya ya kuchonganisha wananchi na serikali yao.Nina mashaka taasisi kama hizi zinatumiwa na baadhi ya vyama vya upinzani ili kuondoa mshikamano na umoja wa kitaifa kwa Watanzania hivyo kuleta vurugu.

Nyambafu..tatizo lenu hamtaki kuambiwa ukweli..mnataka kauli za "uchumi unakua", "ahadi zina tekelezeka" n.k Ninyi ndo mnampoteza dhaifu matokeo yake anaishia na kauli za "nimeambiwa,nimejulishwa" pasipo kuchanganya na zake kama alivyo wadhihaki wafanya kazi kipindi fulani walipotaka kugoma kwa madai wanasikiliza maneno ya kuambiwa ya Mgaya. Sasa naye yame mkuta..
 
Naona mleta mada povu likimtoka! Ukweli ni kwamba hata hizo asilimia 70% za JK na 60% za Bunge ni za kubumba ukilinganisha na hali ilivyo sasa. Laiti utafiti huo ungekuwa umefanywa kwa haki na kuzingatia ukweli bila 'bias' Kikwete asingepata zaidi ya 30% na hili Bunge la vibwetere lisingevuka hata 25%.
Ya kwamba Kikwete na CCM yao wanapendwa na mbumbumbu hilo lilieleweka hata kabla ya kufanyiwa utafiti kwani mtaji wa CCM na viongozi wao ni ujinga wa wapiga kura wanaokubali kuhongwa hata tai wakati hata mashati ya kuvalia hawana! Wapo walio tayari pia kutoa kura kwa kuimbiwa mapambio ya John Komba bila kusahau wasomi wa kati walimu wa shule za msingi ambao kila uchaguzi ukifika 'hukirimiwa' kazi za uwakala na 'kufanikisha' zoezi la upigaji kura kwa kutumika kama punda wa kuwaibia kura. Urafiki wao huwa wa muda mfupi tu, wakishafanikisha CCM huanza kuwanyanyasa hadi uchaguzi mwingine unapokaribia!
Nasisitiza tena na tena umaarufu wa Kikwete umetiwa chumvi na hastahili hata hizo 30%.
 
77% wanompenda prezidaa elimu yao ni chini ya darasa la saba. Na bado....
 
Taasisi kama Afrobarometer ni kikwazo kikubwa katika mustakabali wa taifa letu.Utafiti uchwara wa taasisi hii umekosa mashiko na tija kwa Watanzania.Sidhani ni kweli kwamba mh.Rais Jakaya Kikwete anapendwa na watu wasio kuwa na elimu,na hata kama wakimpenda na kukubali utendaji wake wa kazi kuna tatizo gani?Kwani Watanzania kwa sababu mbalimbali waliokosa elimu hata kama wanampenda rais JK ni utashi wao,taasisi uchwara ya Afrobarometer wanataka hiyo jamii ya waliokosa elimu wampende nani?wampende rais Kagame wa Rwanda?Mh.Rais anapendwa na Watanzania wote,wasomi na wasio wasomi.Sera nzuri za CCM na uwezo mkubwa wa uongozi wa mh.JK vimepelekea Watz wampe ridhaa ya kuongoza taifa letu.Katika kipindi cha uongozi wa JK Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo.Maendeleo ya sasa hivi yameyapita nchi mbalimbali za Afrika.Hivyo taasisi kama Afrobarometer zinatakiwa ziogopwa kama ukoma kwani zinamalengo mabaya ya kuchonganisha wananchi na serikali yao.Nina mashaka taasisi kama hizi zinatumiwa na baadhi ya vyama vya upinzani ili kuondoa mshikamano na umoja wa kitaifa kwa Watanzania hivyo kuleta vurugu.

utafiti hujibiwa kwa utafiti na siyo porojo.....
 
Taasisi kama Afrobarometer ni kikwazo kikubwa katika mustakabali wa taifa letu.Utafiti uchwara wa taasisi hii umekosa mashiko na tija kwa Watanzania.Sidhani ni kweli kwamba mh.Rais Jakaya Kikwete anapendwa na watu wasio kuwa na elimu,na hata kama wakimpenda na kukubali utendaji wake wa kazi kuna tatizo gani?Kwani Watanzania kwa sababu mbalimbali waliokosa elimu hata kama wanampenda rais JK ni utashi wao,taasisi uchwara ya Afrobarometer wanataka hiyo jamii ya waliokosa elimu wampende nani?wampende rais Kagame wa Rwanda?Mh.Rais anapendwa na Watanzania wote,wasomi na wasio wasomi.Sera nzuri za CCM na uwezo mkubwa wa uongozi wa mh.JK vimepelekea Watz wampe ridhaa ya kuongoza taifa letu.Katika kipindi cha uongozi wa JK Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo.Maendeleo ya sasa hivi yameyapita nchi mbalimbali za Afrika.Hivyo taasisi kama Afrobarometer zinatakiwa ziogopwa kama ukoma kwani zinamalengo mabaya ya kuchonganisha wananchi na serikali yao.Nina mashaka taasisi kama hizi zinatumiwa na baadhi ya vyama vya upinzani ili kuondoa mshikamano na umoja wa kitaifa kwa Watanzania hivyo kuleta vurugu.

Mbeyaman,
Kwanza niseme si sahihi hata kidogo kusema Afrobarometer ni taasisi uchwara, janga la taifa au iogopwe kama ukoma eti kwa sababu inalenga kuwachonganisha wananchi na serikali yao. Kimsingi, hiki huwa ni kisingizio kwa serikali karibu zote duniani ambazo hazitekezi matakwa ya wananchi wake na hivyo hazipendi kukosolewa. Kinachowachonganisha wanaserikali yao ni viongozi wa serikali kutotekeza matakwa ya wananchi wao na kuamua kijitumikia wenyewe na chama chao, au kama ambavyo wengine mmezoea kusema sisiemu kwanza. Wananchi je? ni wa pili, tatu au wa mwisho kabisa?

Kwa taarifa yako, Afrobarometer ni taasisi huru ya utafiti yenye watalaam waliobobea kutoka nchi mbalimbali za Afrika na haina mlengo wowote wa kisiasa. Si mara ya kwanza kutoa taarifa za utafiti kama huu. Ilifanya hivyo mwaka 2008 na imeendelea kufanya hivyo katika nchi mbalimbali za Afrika. Tofauti ni kuwa ripoti ya hivi karibuni inaonyesha kugusa baadhi ya mambo hampendi kuyasikia na sishangai kuona unakuja juu kama moto wa kifuu.

Kwa kukusaidia tu ni kuwa utafiti ni taaluma yenye taratibu, misingi na kanuni zake. Huwezi kuibuka tu na kuanza kukataa au kutuhumu watafiti au matokeo ya utafiti fulani kwa sababu tu hayajakufurahisha. Bali unapaswa kuingia kwa undani kidogo ili kufahamu maudhui na namna utafiti huo ulivyofanyika. Ningekuelewa kama ungekuja na maelezo ya kukosoa jinsi utafiti huo ulivyofanyika na hivyo kupelekea matokeo ambayo unafikiri hayatoi picha halisi.

Vinginevyo, kwa sasa, acha propaganda za kisiasa na ukubali tu kuwa hiyo ndiyo hali halisi ya mtazamo wa watanzania kuhusu mihimili ya dola na taasisi zake ikiwemo taasisi ya Rais, mpaka hapo tukapokuwa na ripoti ya utafiti mwingine inaonyesha vinginevyo.
 
Back
Top Bottom