Afrika Kusini wako hatua za mwisho za makubaliano mtambo mkubwa wa umeme wa makaa ya mawe Mbeya

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
12,638
22,490
Kuna wakati humu JF nilitoa ushauri kwa Prof Muhongo kwamba ili kuepukana na tatizo la umeme nchini, aache kabisa kuiingiza Tanzania kwenye mikataba midogo midogo ya uzalishaji umeme chini ya 300MW. Mikataba kama hiyo awaachie watu wa REA. Hata nilimwambia, ukiangalia Afrika Kusini, ni kama wangeweza kutupa umeme wa nchi nzima na ziada kwa kutumia mtambo wao mmoja tu!

Ushauri kwa Prof. Muhongo: Nguvu ya mradi wa Songas hailingani na kinachozalishwa, tusirudie kosa

Labda alinisikia. Sasa hivi Tanzania iko katika hatua za mwisho za makubaliano na kampuni kutoka Afrika Kusini, Kibo Mining, kuelekea kufunga mtambo wa umeme wa makaa ya mawe kule Mbeya wenye uwezo wa kuzalisha umeme wa 250-350MW.

Mtambo huu wa umeme ukikamilika na kuanza kazi, utakuwa ni mtambo wenye kuzalisha umeme mkubwa kuliko yote iliyopo nchini, kutia na ile ya gesi tunayojivunia sana. Itamaanisha mtambo mmoja wa hii kampuni utakuwa unazalisha karibu 30% ya mahitaji ya umeme Tanzania.

Sasa swali ni kwamba, ikiwa kampuni hii inafunga mtambo mmoja tu na tunapata 30% ya umeme unaohitajika nchini, tumeshindwaje kutumia gesi yetu na kuwa na mitambo miwili tu ambayo itazalisha zaidi ya mahitaji yetu ya umeme? Kwa nini tunakuwa na gesi nyingi hivi, na bado tunaingia mikataba ya miradi midogo midogo ya kuzalisha umeme ya uwezo wa 100-150MW, ambayo inatuongezea gharama za mobilization bila sababu za msingi?

Source: African News Agency
Kibo Mining holds talks to accelerate development of Mbeya Coal to Power Project | IOL
 
Hii ni habari njema sana kwetu ila ni habari mbaya zaidi kama hawatasambaza wenyewe na kuwauzia tanesco kwanza
 
Hii ni habari njema sana kwetu ila ni habari mbaya zaidi kama hawatasambaza wenyewe na kuwauzia tanesco kwanza

Mkuu, sidhani sheria iliyounda Tanesco inaruhusu mtu mwingine kusambaza umeme - zaidi ya Tanesco na REA. Kuna wakati tulikuwa tunaongelea "unbundling of the electricity services", ambapo katika umeme kungekuwa uzalishaji, usambazaji na uuzaji (generation, transmission and distribution). Sijui tulifikia wapi na hili. Labda hiyo ingeweka nafasi ya kampuni binafsi kufanya distribution.
 
Mkuu, sidhani sheria iliyounda Tanesco inaruhusu mtu mwingine kusambaza umeme - zaidi ya Tanesco na REA. Kuna wakati tulikuwa tunaongelea "unbundling of the electricity services", ambapo katika umeme kungekuwa uzalishaji, usambazaji na uuzaji (generation, transmission and distribution). Sijui tulifikia wapi na hili. Labda hiyo ingeweka nafasi ya kampuni binafsi kufanya distribution.


Hakika mkuu hili ni tatizo sugu sana.Ukiritimba wa tanesco
 
Kuna wakati humu JF nilitoa ushauri kwa Prof Muhongo kwamba ili kuepukana na tatizo la umeme nchini, na kwa kuwa tuna gesi na makaa ya mawe kwa wingi, aachane kabisa kuiingiza Tanzania kwenye mikataba midoo midogo ya uzalishaji umeme chini ya 200MW. Mikataba kama hiyo awaachie watu wa REA. Hata nilimwambia, ukiangalia Afrika Kusini, ni kama wangeweza kutupa umeme wa nchi nzima na ziada kwa kutumia mitambo yao miwili tu!

Labda alinisikia. Sasa hivi Tanzania iko katika hatua za mwisho za makubaliano na kampuni kutoka Afrika Kusini, Kibo Mining, kuelekea kufunga mtambo wa umeme wa makaa ya mawe kule Mbeya wenye uwezo wa kuzalisha umeme wa 250-350MW.

Mtambo huu wa umeme ukikamilika na kuanza kazi, utakuwa ni mtambo wenye kuzalisha umeme mkubwa kuliko yote iliyopo nchini, kutia na ile ya gesi tunayojivunia sana. Itamaanisha mtambo mmoja wa hii kampuni utakuwa unazalisha karibu 30% ya mahitaji ya umeme Tanzania.

Sasa swali ni kwamba, ikiwa kampuni hii inafunga mtambo mmoja tu na tunapata 30% ya umeme unaohitajika nchini, tumeshindwaje kutumia gesi yetu na kuwa na mitambo miwili tu ambayo itazalisha zaidi ya mahitaji yetu ya umeme? Kwa nini tunakuwa na gesi nyingi hivi, na bado tunaingia mikataba ya miradi midogo midogo ya kuzalisha umeme ya uwezo wa 100-150MW, ambayo inatuongezea gharama za mobilization bila sababu za msingi?

Source: African News Agency
Kibo Mining holds talks to accelerate development of Mbeya Coal to Power Project | IOL
Haya ndo tutamuunga mkono Magu, siyo mbwembwe za Makinikia na ripoti za Mapro Pesa!!!
 
Haya ndo tutamuunga mkono Magu, siyo mbwembwe za Makinikia na ripoti za Mapro Pesa!!!

Na nchi haiwezi kamwe kuwa ya viwanda kama hakuna umeme wa uhakika na bei nafuu, wakati hata ule wa kuwashia taa nyumbani unatupa shida!
 
Jamani hiyo gesi sio yetu! Tukumbuke sio sisi tumeingia chini ya bahari na kuichimba. Tanesco wananunua gesi inayotumika kuendesha mitambo ya kuzalisha umeme.
 
Jamani hiyo gesi sio yetu! Tukumbuke sio sisi tumeingia chini ya bahari na kuichimba. Tanesco wananunua gesi inayotumika kuendesha mitambo ya kuzalisha umeme.


Unajua nilikuwa naangalia signature yako hapa;

"Women=3C'=Cars, Cash, Clothes
Men=3W's=Wine,Wheels,Women"- Scandal

Then you know why any relationship between a man and woman will be mutual - they both end up getting more than they could get on their own - cars, cash, clothes, wine, wheels and each other!

It is always the same things and words that make them complete, just move the comma from here to there

Woman without her man, is nothing
Woman, without her man is nothing
 
Mimi nilishangaa mbwebwe zote za Kinyerezi Phase 1 Megawatt 150 Mpaka saasa Mtera ndio yuko Top ktk power station capacity yake ni 204MW niliwaza Gas patawekwa Genset ya kufua 300MW, Nchi za kuongea nazo juu Umeme ndio hizo sasa SA yuko mbali mno Ethiopia anaetaka kutuuza sijui Anafua MW 5000 tu south ni karibia MW 40000 na ndio ana Nuclear Power station Africa nzima Yeye tu
 
Mkataba unasemaje?
Tusije tukajikuta makaa yetu wao walete mitambo halafu mapato wachukue yote tuwalipe na capacity charges.
Halafu wapandishe na tariffs badala ya kushusha.

MAMBO YOTE IKO KWENYE MKATABA.

Hii ni sawa na kushangilia makinikia.
 
Back
Top Bottom