Kingvictor87
Member
- May 31, 2011
- 83
- 42
habari ya mchana wanajamvi,
Binafsi nimekuwa nizifuatialia sana siasa na diplomasia ya bara la afrika kwa ujumla.
Kumekuwepo na migongano ya hapa na pale baina ya mataifa ya kiafrika na mingi ya migongano hiyo humalizwa kwa kujadiliana kwa pande zinazotofautiana na hatimaye kufikia suluhu. mmoja wa mgogoro wa karibu niukumbukao ni ule baina ya nigeria na south africa ambapo mamlamaka ya uhamiaji ya afrika ya kusini iliwazuia raia wa nigeria kuingia nchini kwao pamoja na kuwa na visa pamoja na documents nyingine zote na kuwarudisha kwao nigeria, baada ya hapo serikali ya nigeria kwa kuwajali wananchi wake ingawa walikuwa ni wachache nao ikawakamata raia wa afrika ya kusini wanaoishi nigeria (inasemekana ni ndege mbili zilijaa)na kuwarudisha kwao johannesburg, baada ya hayo afrika ya kusini iliiomba radhi nigeria na maisha yakaendelea.
sasa nikirudi katika hoja yangu ni kuwa inawezekana kabisa waafrika tukiamua tunaweza, hatuwezi kukaa tukivumilia kuona hali ya ndugu zetu wakichinjwa na kuchomwa moto kama waharifu.hali hii siyo ya kuivumilia kabisa na nimefarijika sana baada ya kuona na kusikia matamko ya baadhi ya nchi za kiafrika kama nigeria ambayo imetoa masaa 24 kwa afrika ya kusini kuwaliza machafuko la sivyo wao watazifunga kampuni za afrika ya kusini zilizopo nchini nigeria, pia serikali ya malawi imetoa usafiri wa kuwarudisha raia wake nyumbani kwao, nasikitishwa sana na utendaji wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa as sijasikia chochote toka kwao mpaka leo nchi ndogo kama malawi inakuwa concerned na wananchi wake kuliko sisi.
maoni yangu juu ya hili linaloendelea kule afrika ya kusini ni kuwa waafrika wengi toka nchi tofauti waliopo kule wanachokipata ni kipato cha kawaida tu kuyamudu maisha tofauti na vipato vikubwa vya makampuni ya afrika ya kusini yanafanya kazi katika nchi tofauti katika bara la afrika(na ikumbukwe kila kampuni ya south africa inalipa kodi pia nchini kwao).
Baadhi ya makumpuni makubwa ambayo yamesambaa barani afrika ni
MTN, Vodacom,FNB Absa (wwamiliki wa NBC),Shoprite, woolworth truworth, multichoice (daily tunalalamika gharama zao) na makampuni ya uchimbaji wa madini turnovers zao kwa mwaka kufanisha kipato wanachopata hao ndugu zetu huko tofauti ni kubwa mno!
so wakiendelea kuwauwa ndugu zetu ni bora na sisi waafrika tukawafukuza hawa wasouth africa waliopo nyumbani kwetu tena wakiendesha sector nono.
asanteni sana
Binafsi nimekuwa nizifuatialia sana siasa na diplomasia ya bara la afrika kwa ujumla.
Kumekuwepo na migongano ya hapa na pale baina ya mataifa ya kiafrika na mingi ya migongano hiyo humalizwa kwa kujadiliana kwa pande zinazotofautiana na hatimaye kufikia suluhu. mmoja wa mgogoro wa karibu niukumbukao ni ule baina ya nigeria na south africa ambapo mamlamaka ya uhamiaji ya afrika ya kusini iliwazuia raia wa nigeria kuingia nchini kwao pamoja na kuwa na visa pamoja na documents nyingine zote na kuwarudisha kwao nigeria, baada ya hapo serikali ya nigeria kwa kuwajali wananchi wake ingawa walikuwa ni wachache nao ikawakamata raia wa afrika ya kusini wanaoishi nigeria (inasemekana ni ndege mbili zilijaa)na kuwarudisha kwao johannesburg, baada ya hayo afrika ya kusini iliiomba radhi nigeria na maisha yakaendelea.
sasa nikirudi katika hoja yangu ni kuwa inawezekana kabisa waafrika tukiamua tunaweza, hatuwezi kukaa tukivumilia kuona hali ya ndugu zetu wakichinjwa na kuchomwa moto kama waharifu.hali hii siyo ya kuivumilia kabisa na nimefarijika sana baada ya kuona na kusikia matamko ya baadhi ya nchi za kiafrika kama nigeria ambayo imetoa masaa 24 kwa afrika ya kusini kuwaliza machafuko la sivyo wao watazifunga kampuni za afrika ya kusini zilizopo nchini nigeria, pia serikali ya malawi imetoa usafiri wa kuwarudisha raia wake nyumbani kwao, nasikitishwa sana na utendaji wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa as sijasikia chochote toka kwao mpaka leo nchi ndogo kama malawi inakuwa concerned na wananchi wake kuliko sisi.
maoni yangu juu ya hili linaloendelea kule afrika ya kusini ni kuwa waafrika wengi toka nchi tofauti waliopo kule wanachokipata ni kipato cha kawaida tu kuyamudu maisha tofauti na vipato vikubwa vya makampuni ya afrika ya kusini yanafanya kazi katika nchi tofauti katika bara la afrika(na ikumbukwe kila kampuni ya south africa inalipa kodi pia nchini kwao).
Baadhi ya makumpuni makubwa ambayo yamesambaa barani afrika ni
MTN, Vodacom,FNB Absa (wwamiliki wa NBC),Shoprite, woolworth truworth, multichoice (daily tunalalamika gharama zao) na makampuni ya uchimbaji wa madini turnovers zao kwa mwaka kufanisha kipato wanachopata hao ndugu zetu huko tofauti ni kubwa mno!
so wakiendelea kuwauwa ndugu zetu ni bora na sisi waafrika tukawafukuza hawa wasouth africa waliopo nyumbani kwetu tena wakiendesha sector nono.
asanteni sana