Afrika inakwenda kombo-tujimumushe

Afrika inakwenda kombo-tujimumushe

mwankuga

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2010
Posts
334
Reaction score
120
Mwaka 1962,Mfaransa R.DUMONT aliandika kitabu kiitwacho THE FALSE START OF AFRICA,ambacho kimefupishwa na kutafsiriwa na GABRIEL RUHUMBIKA mwaka 1974.Katika dibaji ya kitabu hicho kinasema hivi;"Afrika inakwenda kombo!Jina la kitabu chako ni kali sana.Kitawakasirisha Waafrika.Unafahamu jinsi wasivyopenda kutolewa makosa.Utasemwa kama unawanyanyasa kama mkoloni mwenyewe;kwani kuyatoa makosa mataifa mapya haya na viongozi wake ni kuunga mkono,waliokuwa wakidai kwamba Waafrika hawajawa tayari kujitawala".

UKURASA WA 39."WATEULE WANAISHI KAMA MTOTO WA MFALME.
"Haiwezekani kuendeleza nchi kwa kuongeza maradufu wafanyakazi wa ofisini au kwa kugawia marafiki vyeovinavyowapatia mishahara bila kufanya kazi,ila tu kwa kuunganisha watu wenye utashi wa kazi ili kutekeleza matakwa yanayomfaidisha kila mmoja.Kama mambo yasiporekebishwa,uendeshaji wa serikali ndio utakaoteketeza nchi za Kiafrika".

"Kwa waziri mdogo ana motokaa ya serikali ambayo mara nyingi si motokaa ndogo,pamoja na dereva,kwa matumizi yake binafsi.Raisi wa nchi ndogo kama Dahomey hawezi kutoka nje bila kutanguliwa na safu za za askari wa pikipiki,na wengi wa hawa maraisi wanaota kushindana na ikulu ya Ufaransa."pg 40

"Wafanya kazi wa serikali,wabunge na mawaziri wameunda kundi lililoneemeka sana na linalojijali lenyewe peke yake.Uingereza mbunge anapata mshahara wa mtumishi wa cheo cha kati.Ufaransa anapata ule mshahara wa cheo cha juu.Kwa sababu ya ile siasa ya UZUNGU MWEUSI ilitaka makoloni ya Wafaransa yaamini kuwa na yenyewe pia ni Ufaransa,mbunge wa nchi ndogo sana na masikini kama Gaboni anapokea mshahara mkubwa kuliko wa mbunge wa Kiingereza"

"Maraisi na mawaziri wajanja wanarundika akiba kwa siku za uzee katika mabenki ya Switzerland,na wake zao wananunua majumba makubwa makubwa kandokando ya ziwa Geneva huko huko Switzerland"pg 41.

"Awe mbunge au mtumishi wa serikali,mara tu Mwaafrika akisha pata anaona lazima ndugu zake,siku nyingine kijiji chake chote,nao wafaidi.Ukarimu ambao ni jadi ya Waafrika unastahili sifa unapomaanisha tuseme mtu kumwelimisha mpwa wake masikini mpaka kufikia kumaliza masomo yake"pg44

"Maofisini nafasi nyingi sana za kazi zinajazwa kwa kufuata undugu,na sio ujuzi wa kazi.Mkubwa wa ofisi ya waziri kwa kawaida ni mtu wa kabila la waziri yule.Maofisa hasa mawaziri wanapoteza vibaya sana muda wao wa nadra,ambao wangeweza kutumia kusoma ripoti za wizara zao au ktembelea sehemu zilizo na matatizo na kuyachunguza".

Ngoja niishie hapo,lakini inasemekana kuwa Hayati J.K Nyerere amewahi kuwalazimisha waziri kukisoma kitabu hicho kwani kimefichua tabia nyingi ambazo Waafrika wamerithi kutoka kwa wakoloni.

Naipost thread hii ili kutaka kuwahamasisha wana jamii kujenga utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali.Pia naomba mkitafuta kitabu hicho,kwa sababu ya tabia hizi za viongozi wetu kutaka ufahari,maisha ya peponi,matanuzi ya kutisha tofauti na maisha ya wananchi waliowengi.Kimsingi tuna matatizo mengi sana ambayo ni lazima tushikamane kwa upendo kukatisha ndoa ya viongozi wetu na mafisadi.Hawa viongozi wetu ni hatari sana kuliko tunavyoana.

Nasubiri mrejesho kutoka kwenu wadau,baada ya hapo tutakuja kwenye maisha ya sasa ya viongozi wetu kwa kusema mambo maovu na pasipo kujali.Naomba kuwasilisha.
 
Nakubaliana na wewe mkuu! This is a true color ya utawala wa kiafrika na halina ubishi hata chembe. anayebishi na seme sasa tumuone. copy ya hicho kitabu twaweza kuipata wapi? Soma na kile cha ''it's our turn to eat'' cha wakenya humo pia utajionea tabia halisi ya wakoloni weusi!
 
Nakubaliana na wewe mkuu! This is a true color ya utawala wa kiafrika na halina ubishi hata chembe. anayebishi na seme sasa tumuone. copy ya hicho kitabu twaweza kuipata wapi? Soma na kile cha ''it's our turn to eat'' cha wakenya humo pia utajionea tabia halisi ya wakoloni weusi!

Mkuu nitajitahidi kukitafuta kitabu hicho,kuhusu kitabu cha "THE FALSE START OF AFRICA" kinaweza kupatikana katika bookshop ya UDSM.
 
Kwa bahati mbaya au nzuri nilikisoma kitabu hicho nikiwa darasa la pili kikanichanganya akili nikaichukia hali ya kisiasa ya Afrika hata sasa. Ukisoma maelezo yake kinasema hata Nyerere aliwalazimisha mawaziri wake wote wakisome na kukielewa kitabu kile. Nahisi ni Nyerere aliyelipia ile tafsiri ya kiswahili ya babu yangu Ruhumbika. Jamani sio siri, Afrika inakwenda kombo na hasa Tanzania.
 
sudan zinajitenga kuwa inchi mbili sasa zanzibar nayo ina fuatia nadhani wanhaki ya kuwa huru
 
sudan zinajitenga kuwa inchi mbili sasa zanzibar nayo ina fuatia nadhani wanhaki ya kuwa huru

Ninaitamani siku tutakayojitenga na Zanzibar.....................na ije siku hiyo mapema.
 
Mwaka 1962,Mfaransa R.DUMONT aliandika kitabu kiitwacho THE FALSE START OF AFRICA,ambacho kimefupishwa na kutafsiriwa na GABRIEL RUHUMBIKA mwaka 1974.Katika dibaji ya kitabu hicho kinasema hivi;" Afrika inakwenda kombo!Jina la kitabu chako ni kali sana.Kitawakasirisha Waafrika.Unafahamu jinsi wasivyopenda kutolewa makosa.Utasemwa kama unawanyanyasa kama mkoloni mwenyewe;kwani kuyatoa makosa mataifa mapya haya na viongozi wake ni kuunga mkono,waliokuwa wakidai kwamba Waafrika hawajawa tayari kujitawala".

UKURASA WA 39."WATEULE WANAISHI KAMA MTOTO WA MFALME.
"Haiwezekani kuendeleza nchi kwa kuongeza maradufu wafanyakazi wa ofisini au kwa kugawia marafiki vyeovinavyowapatia mishahara bila kufanya kazi,ila tu kwa kuunganisha watu wenye utashi wa kazi ili kutekeleza matakwa yanayomfaidisha kila mmoja.Kama mambo yasiporekebishwa,uendeshaji wa serikali ndio utakaoteketeza nchi za Kiafrika".

"Kwa waziri mdogo ana motokaa ya serikali ambayo mara nyingi si motokaa ndogo,pamoja na dereva,kwa matumizi yake binafsi.Raisi wa nchi ndogo kama Dahomey hawezi kutoka nje bila kutanguliwa na safu za za askari wa pikipiki,na wengi wa hawa maraisi wanaota kushindana na ikulu ya Ufaransa."pg 40

"Wafanya kazi wa serikali,wabunge na mawaziri wameunda kundi lililoneemeka sana na linalojijali lenyewe peke yake. Uingereza mbunge anapata mshahara wa mtumishi wa cheo cha kati.Ufaransa anapata ule mshahara wa cheo cha juu.Kwa sababu ya ile siasa ya UZUNGU MWEUSI ilitaka makoloni ya Wafaransa yaamini kuwa na yenyewe pia ni Ufaransa,mbunge wa nchi ndogo sana na masikini kama Gaboni anapokea mshahara mkubwa kuliko wa mbunge wa Kiingereza"

"Maraisi na mawaziri wajanja wanarundika akiba kwa siku za uzee katika mabenki ya Switzerland,na wake zao wananunua majumba makubwa makubwa kandokando ya ziwa Geneva huko huko Switzerland "pg 41.

"Awe mbunge au mtumishi wa serikali,mara tu Mwaafrika akisha pata anaona lazima ndugu zake,siku nyingine kijiji chake chote,nao wafaidi .Ukarimu ambao ni jadi ya Waafrika unastahili sifa unapomaanisha tuseme mtu kumwelimisha mpwa wake masikini mpaka kufikia kumaliza masomo yake"pg44

"Maofisini nafasi nyingi sana za kazi zinajazwa kwa kufuata undugu,na sio ujuzi wa kazi. Mkubwa wa ofisi ya waziri kwa kawaida ni mtu wa kabila la waziri yule.Maofisa hasa mawaziri wanapoteza vibaya sana muda wao wa nadra,ambao wangeweza kutumia kusoma ripoti za wizara zao au ktembelea sehemu zilizo na matatizo na kuyachunguza".

Ngoja niishie hapo,lakini inasemekana kuwa Hayati J.K Nyerere amewahi kuwalazimisha waziri kukisoma kitabu hicho kwani kimefichua tabia nyingi ambazo Waafrika wamerithi kutoka kwa wakoloni.

Naipost thread hii ili kutaka kuwahamasisha wana jamii kujenga utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali.Pia naomba mkitafuta kitabu hicho,kwa sababu ya tabia hizi za viongozi wetu kutaka ufahari,maisha ya peponi,matanuzi ya kutisha tofauti na maisha ya wananchi waliowengi.Kimsingi tuna matatizo mengi sana ambayo ni lazima tushikamane kwa upendo kukatisha ndoa ya viongozi wetu na mafisadi.Hawa viongozi wetu ni hatari sana kuliko tunavyoana.

Nasubiri mrejesho kutoka kwenu wadau,baada ya hapo tutakuja kwenye maisha ya sasa ya viongozi wetu kwa kusema mambo maovu na pasipo kujali.Naomba kuwasilisha.

Maneno aliyoandika Rene' Dumont miaka ya sitini, yakajidhihiri kwa ufasaha katika tawala za kiafrika. Miaka imeenda ikarudi, ikaingia demokrasia na vyama vingi huku vyama vya upinzani vikijinadi kuleta ukombozi na kubadilisha hali hiyo, leo hii natafakari kwa kina kujaribu kuiona tofauti lakini sioni, zaidi tu sana inadhihirika kuwa hata tunaojaribu kuwaamini kuwa wanahubiri mabadiliko, mapinduzi na ukombozi nao ni walewale, wanatusukuma kwenye mwanzo ule ule mbovu wa Afrika. Ama niseme tu mara hii kwamba, ''Tanzania inakwenda kombo''
 
Mwaka 1962,Mfaransa R.DUMONT aliandika kitabukiitwacho THE FALSE START OF AFRICA,ambacho kimefupishwa na kutafsiriwa naGABRIEL RUHUMBIKA mwaka 1974.Katika dibaji ya kitabu hicho kinasema hivi;" Afrikainakwenda kombo!Jina la kitabu chako ni kali sana.Kitawakasirisha Waafrika.Unafahamujinsi wasivyopenda kutolewa makosa . Utasemwa kama unawanyanyasa kama mkoloni mwenyewe;kwani kuyatoa makosamataifa mapya haya na viongozi wake ni kuunga mkono,waliokuwa wakidai kwambaWaafrika hawajawa tayari kujitawala".

UKURASA WA 39."WATEULE WANAISHIKAMA MTOTO WA MFALME.
"Haiwezekani kuendeleza nchikwa kuongeza maradufu wafanyakazi wa ofisini au kwa kugawia marafikivyeovinavyowapatia mishahara bila kufanya kazi,ila tu kwa kuunganisha watuwenye utashi wa kazi ili kutekeleza matakwa yanayomfaidisha kila mmoja.Kamamambo yasiporekebishwa,uendeshaji wa serikali ndio utakaoteketeza nchi zaKiafrika".

"Kwa waziri mdogo ana motokaa ya serikaliambayo mara nyingi si motokaa ndogo,pamoja na dereva,kwa matumizi yake binafsi. Raisi wa nchi ndogo kama Dahomey hawezikutoka nje bila kutanguliwa na safu za za askari wa pikipiki,na wengi wa hawamaraisi wanaota kushindana na ikulu ya Ufaransa."pg 40

"Wafanya kazi wa serikali,wabunge namawaziri wameunda kundi lililoneemeka sana na linalojijali lenyewe peke yake. Uingerezambunge anapata mshahara wa mtumishi wa cheo cha kati.Ufaransa anapata ulemshahara wa cheo cha juu.Kwa sababu ya ile siasa ya UZUNGU MWEUSI ilitakamakoloni ya Wafaransa yaamini kuwa na yenyewe pia ni Ufaransa,mbunge wa nchindogo sana na masikini kama Gaboni anapokea mshahara mkubwa kuliko wa mbunge waKiingereza"

"Maraisi na mawaziri wajanja wanarundikaakiba kwa siku za uzee katika mabenki ya Switzerland,na wake zao wananunuamajumba makubwa makubwa kandokando ya ziwa Geneva huko huko Switzerland "pg 41.

"Awe mbunge au mtumishi wa serikali,maratu Mwaafrika akisha pata anaona lazima ndugu zake,siku nyingine kijiji chakechote,nao wafaidi . Ukarimu ambao ni jadi ya Waafrikaunastahili sifa unapomaanisha tuseme mtu kumwelimisha mpwa wake masikini mpakakufikia kumaliza masomo yake"pg44

"Maofisini nafasi nyingi sana za kazizinajazwa kwa kufuata undugu,na sio ujuzi wa kazi. Mkubwa wa ofisi ya wazirikwa kawaida ni mtu wa kabila la waziri yule. Maofisa hasa mawaziri wanapoteza vibayasana muda wao wa nadra,ambao wangeweza kutumia kusoma ripoti za wizara zao auktembelea sehemu zilizo na matatizo na kuyachunguza".

Ngoja niishie hapo,lakiniinasemekana kuwa Hayati J.K Nyerere amewahi kuwalazimisha waziri kukisomakitabu hicho kwani kimefichua tabia nyingi ambazo Waafrika wamerithi kutoka kwawakoloni.

Naipost thread hii ili kutakakuwahamasisha wana jamii kujenga utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali.Pianaomba mkitafuta kitabu hicho,kwa sababu ya tabia hizi za viongozi wetu kutakaufahari,maisha ya peponi,matanuzi ya kutisha tofauti na maisha ya wananchiwaliowengi.Kimsingi tuna matatizo mengi sana ambayo ni lazima tushikamane kwaupendo kukatisha ndoa ya viongozi wetu na mafisadi.Hawa viongozi wetu ni hatarisana kuliko tunavyoana.

Nasubiri mrejesho kutoka kwenuwadau,baada ya hapo tutakuja kwenye maisha ya sasa ya viongozi wetu kwa kusemamambo maovu na pasipo kujali.Naomba kuwasilisha.


Maneno aliyoandika Rene' Dumont miaka ya sitini, yakajidhihiri kwa ufasahakatika tawala za kiafrika. Miaka imeenda ikarudi, ikaingia demokrasia na vyamavingi huku vyama vya upinzani vikijinadi kuleta ukombozi na kubadilisha halihiyo, leo hii natafakari kwa kina kujaribu kuiona tofauti lakini sioni, zaidi tusana inadhihirika kuwa hata tunaojaribu kuwaamini kuwa wanahubiri mabadiliko,mapinduzi na ukombozi nao ni walewale, wanatusukuma kwenye mwanzo ule ule mbovuwa Afrika. Ama niseme tu mara hii kwamba, ''Tanzania inakwenda kombo''

 
Back
Top Bottom