mwankuga
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 334
- 120
Mwaka 1962,Mfaransa R.DUMONT aliandika kitabu kiitwacho THE FALSE START OF AFRICA,ambacho kimefupishwa na kutafsiriwa na GABRIEL RUHUMBIKA mwaka 1974.Katika dibaji ya kitabu hicho kinasema hivi;"Afrika inakwenda kombo!Jina la kitabu chako ni kali sana.Kitawakasirisha Waafrika.Unafahamu jinsi wasivyopenda kutolewa makosa.Utasemwa kama unawanyanyasa kama mkoloni mwenyewe;kwani kuyatoa makosa mataifa mapya haya na viongozi wake ni kuunga mkono,waliokuwa wakidai kwamba Waafrika hawajawa tayari kujitawala".
UKURASA WA 39."WATEULE WANAISHI KAMA MTOTO WA MFALME.
"Haiwezekani kuendeleza nchi kwa kuongeza maradufu wafanyakazi wa ofisini au kwa kugawia marafiki vyeovinavyowapatia mishahara bila kufanya kazi,ila tu kwa kuunganisha watu wenye utashi wa kazi ili kutekeleza matakwa yanayomfaidisha kila mmoja.Kama mambo yasiporekebishwa,uendeshaji wa serikali ndio utakaoteketeza nchi za Kiafrika".
"Kwa waziri mdogo ana motokaa ya serikali ambayo mara nyingi si motokaa ndogo,pamoja na dereva,kwa matumizi yake binafsi.Raisi wa nchi ndogo kama Dahomey hawezi kutoka nje bila kutanguliwa na safu za za askari wa pikipiki,na wengi wa hawa maraisi wanaota kushindana na ikulu ya Ufaransa."pg 40
"Wafanya kazi wa serikali,wabunge na mawaziri wameunda kundi lililoneemeka sana na linalojijali lenyewe peke yake.Uingereza mbunge anapata mshahara wa mtumishi wa cheo cha kati.Ufaransa anapata ule mshahara wa cheo cha juu.Kwa sababu ya ile siasa ya UZUNGU MWEUSI ilitaka makoloni ya Wafaransa yaamini kuwa na yenyewe pia ni Ufaransa,mbunge wa nchi ndogo sana na masikini kama Gaboni anapokea mshahara mkubwa kuliko wa mbunge wa Kiingereza"
"Maraisi na mawaziri wajanja wanarundika akiba kwa siku za uzee katika mabenki ya Switzerland,na wake zao wananunua majumba makubwa makubwa kandokando ya ziwa Geneva huko huko Switzerland"pg 41.
"Awe mbunge au mtumishi wa serikali,mara tu Mwaafrika akisha pata anaona lazima ndugu zake,siku nyingine kijiji chake chote,nao wafaidi.Ukarimu ambao ni jadi ya Waafrika unastahili sifa unapomaanisha tuseme mtu kumwelimisha mpwa wake masikini mpaka kufikia kumaliza masomo yake"pg44
"Maofisini nafasi nyingi sana za kazi zinajazwa kwa kufuata undugu,na sio ujuzi wa kazi.Mkubwa wa ofisi ya waziri kwa kawaida ni mtu wa kabila la waziri yule.Maofisa hasa mawaziri wanapoteza vibaya sana muda wao wa nadra,ambao wangeweza kutumia kusoma ripoti za wizara zao au ktembelea sehemu zilizo na matatizo na kuyachunguza".
Ngoja niishie hapo,lakini inasemekana kuwa Hayati J.K Nyerere amewahi kuwalazimisha waziri kukisoma kitabu hicho kwani kimefichua tabia nyingi ambazo Waafrika wamerithi kutoka kwa wakoloni.
Naipost thread hii ili kutaka kuwahamasisha wana jamii kujenga utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali.Pia naomba mkitafuta kitabu hicho,kwa sababu ya tabia hizi za viongozi wetu kutaka ufahari,maisha ya peponi,matanuzi ya kutisha tofauti na maisha ya wananchi waliowengi.Kimsingi tuna matatizo mengi sana ambayo ni lazima tushikamane kwa upendo kukatisha ndoa ya viongozi wetu na mafisadi.Hawa viongozi wetu ni hatari sana kuliko tunavyoana.
Nasubiri mrejesho kutoka kwenu wadau,baada ya hapo tutakuja kwenye maisha ya sasa ya viongozi wetu kwa kusema mambo maovu na pasipo kujali.Naomba kuwasilisha.
UKURASA WA 39."WATEULE WANAISHI KAMA MTOTO WA MFALME.
"Haiwezekani kuendeleza nchi kwa kuongeza maradufu wafanyakazi wa ofisini au kwa kugawia marafiki vyeovinavyowapatia mishahara bila kufanya kazi,ila tu kwa kuunganisha watu wenye utashi wa kazi ili kutekeleza matakwa yanayomfaidisha kila mmoja.Kama mambo yasiporekebishwa,uendeshaji wa serikali ndio utakaoteketeza nchi za Kiafrika".
"Kwa waziri mdogo ana motokaa ya serikali ambayo mara nyingi si motokaa ndogo,pamoja na dereva,kwa matumizi yake binafsi.Raisi wa nchi ndogo kama Dahomey hawezi kutoka nje bila kutanguliwa na safu za za askari wa pikipiki,na wengi wa hawa maraisi wanaota kushindana na ikulu ya Ufaransa."pg 40
"Wafanya kazi wa serikali,wabunge na mawaziri wameunda kundi lililoneemeka sana na linalojijali lenyewe peke yake.Uingereza mbunge anapata mshahara wa mtumishi wa cheo cha kati.Ufaransa anapata ule mshahara wa cheo cha juu.Kwa sababu ya ile siasa ya UZUNGU MWEUSI ilitaka makoloni ya Wafaransa yaamini kuwa na yenyewe pia ni Ufaransa,mbunge wa nchi ndogo sana na masikini kama Gaboni anapokea mshahara mkubwa kuliko wa mbunge wa Kiingereza"
"Maraisi na mawaziri wajanja wanarundika akiba kwa siku za uzee katika mabenki ya Switzerland,na wake zao wananunua majumba makubwa makubwa kandokando ya ziwa Geneva huko huko Switzerland"pg 41.
"Awe mbunge au mtumishi wa serikali,mara tu Mwaafrika akisha pata anaona lazima ndugu zake,siku nyingine kijiji chake chote,nao wafaidi.Ukarimu ambao ni jadi ya Waafrika unastahili sifa unapomaanisha tuseme mtu kumwelimisha mpwa wake masikini mpaka kufikia kumaliza masomo yake"pg44
"Maofisini nafasi nyingi sana za kazi zinajazwa kwa kufuata undugu,na sio ujuzi wa kazi.Mkubwa wa ofisi ya waziri kwa kawaida ni mtu wa kabila la waziri yule.Maofisa hasa mawaziri wanapoteza vibaya sana muda wao wa nadra,ambao wangeweza kutumia kusoma ripoti za wizara zao au ktembelea sehemu zilizo na matatizo na kuyachunguza".
Ngoja niishie hapo,lakini inasemekana kuwa Hayati J.K Nyerere amewahi kuwalazimisha waziri kukisoma kitabu hicho kwani kimefichua tabia nyingi ambazo Waafrika wamerithi kutoka kwa wakoloni.
Naipost thread hii ili kutaka kuwahamasisha wana jamii kujenga utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali.Pia naomba mkitafuta kitabu hicho,kwa sababu ya tabia hizi za viongozi wetu kutaka ufahari,maisha ya peponi,matanuzi ya kutisha tofauti na maisha ya wananchi waliowengi.Kimsingi tuna matatizo mengi sana ambayo ni lazima tushikamane kwa upendo kukatisha ndoa ya viongozi wetu na mafisadi.Hawa viongozi wetu ni hatari sana kuliko tunavyoana.
Nasubiri mrejesho kutoka kwenu wadau,baada ya hapo tutakuja kwenye maisha ya sasa ya viongozi wetu kwa kusema mambo maovu na pasipo kujali.Naomba kuwasilisha.