Africa Kwenye mikutano ya G8/G7

Africa Kwenye mikutano ya G8/G7

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,824
Reaction score
24,481
G7 na kikundi cha nchi zinazjiita zenye viwanda sana, ingawa kwa leo madai hayo siyo sahihi sana kwani India, China na Brazili pia zina viwanda sana. Kikundi hiki kianza mwaka 1974 wakati wa mgogor wa mafuta. baadaye mwaka 1998, Bill Clinton Tonny Blair wakamkaribisha Boris yelstin wa Russia kujiunga na kikundi hicho ingawa uchumi wa Russia haukuwa wa juu kulingana na wanachama wengine, na hivyo kubadili jina kuwa G8. Kutokana na Russia kukamata kwa nguvu peninsula ya Crimea mwaka 2014, ilifukuzwa kutoka kwenye kundi hilo na kurudia kuwa G7.

katika miaka 45 ya uhai wa kikundi hicho, viongozi wa nchi hizo hukuna mara moja kwa mwaka kwenye mkutanoa wanaouita G8 Summit/G7 Summit. Kuanzia mwaka 2002,viongozi hao G8/G7 hualika viongozi wa nchi nyingine ambazo siyo wanachama wa G7 ama kama invited guests au limited invited guests. Katika kipindi hicho cha miaka 16, kwa afrika nchi zilzowahi kualikwa ni kama ifuatavyo:

South Africa (12), Senegal (10), Nigeria (8),Ethiopia(7), Algeria (6), Egypt(5),Kenya (2),Ghana(2), Rwanda (2), Uganda (1), Tanzania(1), Liberia(1), Libya(1), Angola(1), Malawi (1), Tunisia(1), Guinea(1), Niger(1), Seychells(1), Chad(1).

Mwaka 2016 ni Chad tu ndiyo iliyokaribishwa wakati mwaka 2006 ni SA tu ndiyo iliyokaribishwa.

Je frequency ya kuhudhuria mikutano hiyo ni proportional na viwanda ndani ya nchi husika? Naona South Afrika iko kama member kwa sababu wamekosa mituno hiyo michache sana, Tanzania ilihudhuria mkutano wa mwaka 2008 huko Japan kama Limited Guest Invitee, siyo invited Guest.

Tukomae zaidi na viwanda ili nasi tuheshimike kwenye kikundi hicho?
 
Faida yake ni nini? kama wanakwenda kugonga tu wisky maana kwa miaka yote hyo huwezi sema ni nchi 7 tu zimeendelea kumiliki viwanda peke yao ,ili takiwa kwa sasa iwe imefikia angalau G12 na syo G7 miaka yote hyo.
 
Faida yake ni nini? kama wanakwenda kugonga tu wisky maana kwa miaka yote hyo huwezi sema ni nchi 7 tu zimeendelea kumiliki viwanda peke yao ,ili takiwa kwa sasa iwe imefikia angalau G12 na syo G7 miaka yote hyo.
Zamani kidogo walikuwa wanajadili mambo makubwa ya uchumi wa dunia, nakumbuka wakati wa Clinton na Tonny Blair waliwahi kujadili jinsi ya kusaidi nchi za dunia ya tatu kuondokana na umaskini. Lakini siku hizi sidhani kama wanafanya la maana tena; labda Trump akimaliza muda wake
 
Zamani kidogo walikuwa wanajadili mambo makubwa ya uchumi wa dunia, nakumbuka wakati wa Clinton na Tonny Blair waliwahi kujadili jinsi ya kusaidi nchi za dunia ya tatu kuondokana na umaskini. Lakini siku hizi sidhani kama wanafanya la maana tena; labda Trump akimaliza muda wake
Ndgu hawa jamaa kwa sasa wanatuangalia kama soko la kuuzia bidhaa zao na kupata malighafi kama madini yetu kuendeleza viwanda vyao kama vya kutengeneza simu ,hivyo tukiendelea pia masoko ya bidhaa zao yatapungua
 
Tukomae zaidi na viwanda ili nasi tuheshimike kwenye kikundi hicho?
Hicho ni kikundi cha waporaji na wanyonyaji wa rasilimali za nchi changa ili kuneemesha mataifa yao.Hawawezi kumheshimu yoyote zaidi ya wao wenyewe.
 
Trump amesema "hakuna haja ya kujadili maendeleo ya africa "kwa sababu ni mada isiyo na maana.
Ebola na majanga mengine ya Africa kwa Trump hakuna maana maana anatambua kuwa ukitoa msaada wa elimu $bil1 ukagawa Jiwe atapeleka kwenye SGR halafu anasema ni pesa Cash kumbe za mabeberu
 
Trump amesema "hakuna haja ya kujadili maendeleo ya africa "kwa sababu ni mada isiyo na maana.
Ebola na majanga mengine ya Africa kwa Trump hakuna maana maana anatambua kuwa ukitoa msaada wa elimu $bil1 ukagawa Jiwe atapeleka kwenye SGR halafu anasema ni pesa Cash kumbe za mabeberu
Hapo mwisho umegongelea bonge la msumari 😂😂😂
Nalog off
 
Trump amesema "hakuna haja ya kujadili maendeleo ya africa "kwa sababu ni mada isiyo na maana.
Ebola na majanga mengine ya Africa kwa Trump hakuna maana maana anatambua kuwa ukitoa msaada wa elimu $bil1 ukagawa Jiwe atapeleka kwenye SGR halafu anasema ni pesa Cash kumbe za mabeberu
Huyu jamaa kichwa maji sana yaani! Haitoshi,.. wadau wa maendeleo Tanzania wanajiondoa na Watanzania wengi walio ajiriwa na taasisi hizo wanazidi kupoteza ajira kila siku sababu ya upumbavu huu.

Sifa za kijinga tuu!

Magu🚮🚮🚮
 
Back
Top Bottom