Kwa masikitiko makubwa napenda kuufahamisha umma wa watz, tabia za Afisa huyu ambae kwa kweli anacheza na mitaji yetu wafanyabiashara wa mazao ya misitu tunaofanya biashara katika wilaya hii.
Kwa makusudi kabisa hataki kuitisha kikao cha wilaya cha kujadili maombi ya leseni. Tumetuma maombi hayo tangu mwezi Julai mwaka jana, tumelipia usajili hadi sasa unakaribia kuisha mwezi june mwaka huu. Kibaya zaidi tunapompigia kuuliza ni lini anatujibu vibaya kwa kejeli na dharau.
Kabla uvunaji ulikuwa unasimamiwa naye mambo yalikuwa yanaenda vizuri, pesa ikitumwa toka wizarani anatutaarifu pesa tayari leteni maombi. Sasa pesa ipo lakini haiti vikao kwa kuwa wizi alokuwa anafanya na baadhi ya wafanyabiashara sasa hivi amedhibitiwa. Rungu liko na watu wa wizara husika. Matokeo anatutesa wafanyabiashara ambao tunalipa kodi zetu na zimeenda bure. Afisa huyu amesababisha wafanyabiashara wengi sana kukimbia mpanda kutokana na ubabe wake. Ana wafanyabiashara wake ambao imefika mahali anapanda malori yao yenye mbao na kuwasindikiza hadi Sumbawanga wakiwa hawana vibali, yeye ndio anakuwa kibali. Pia anatumia watumishi walio chini yake kutunyanyasa wafanyabiashara, mfano kuna mfanyakazi alimwachia ofisi kipindi yupo masomoni katusumbua na kutufilisi sana pale tulipokataa kutoa pesa za kumpa ampelekee bosi wake. Uongozi wa mkoa wa katavi unalijua hili ila unalifumbia macho, kwa kuwa tumepeleka sana malalamiko kwa mkurugenzi wa Halmashauri wa kipindi cha nyuma ambae sasa hivi ni RAS wa Katavi. Lakini hajafanya lolote. Hivi nchi hii tutawaabudu watu kama hawa hadi lini? Huyu ni mtu mdogo sana hawezi kusema ana kazi nyingi kipindi chote cha miezi takriban kumi. Kama kabla ilikuwa inawezekana, kwa nini sasa hivi inakuwa ngumu?
Kwa makusudi kabisa hataki kuitisha kikao cha wilaya cha kujadili maombi ya leseni. Tumetuma maombi hayo tangu mwezi Julai mwaka jana, tumelipia usajili hadi sasa unakaribia kuisha mwezi june mwaka huu. Kibaya zaidi tunapompigia kuuliza ni lini anatujibu vibaya kwa kejeli na dharau.
Kabla uvunaji ulikuwa unasimamiwa naye mambo yalikuwa yanaenda vizuri, pesa ikitumwa toka wizarani anatutaarifu pesa tayari leteni maombi. Sasa pesa ipo lakini haiti vikao kwa kuwa wizi alokuwa anafanya na baadhi ya wafanyabiashara sasa hivi amedhibitiwa. Rungu liko na watu wa wizara husika. Matokeo anatutesa wafanyabiashara ambao tunalipa kodi zetu na zimeenda bure. Afisa huyu amesababisha wafanyabiashara wengi sana kukimbia mpanda kutokana na ubabe wake. Ana wafanyabiashara wake ambao imefika mahali anapanda malori yao yenye mbao na kuwasindikiza hadi Sumbawanga wakiwa hawana vibali, yeye ndio anakuwa kibali. Pia anatumia watumishi walio chini yake kutunyanyasa wafanyabiashara, mfano kuna mfanyakazi alimwachia ofisi kipindi yupo masomoni katusumbua na kutufilisi sana pale tulipokataa kutoa pesa za kumpa ampelekee bosi wake. Uongozi wa mkoa wa katavi unalijua hili ila unalifumbia macho, kwa kuwa tumepeleka sana malalamiko kwa mkurugenzi wa Halmashauri wa kipindi cha nyuma ambae sasa hivi ni RAS wa Katavi. Lakini hajafanya lolote. Hivi nchi hii tutawaabudu watu kama hawa hadi lini? Huyu ni mtu mdogo sana hawezi kusema ana kazi nyingi kipindi chote cha miezi takriban kumi. Kama kabla ilikuwa inawezekana, kwa nini sasa hivi inakuwa ngumu?