bona
JF-Expert Member
- Nov 6, 2009
- 3,798
- 1,435
wana JF leo tumjadili director of public prosecution ndugu eliaza feleshi, wengi wetu tunailaumu pccb kua haiwachunguzi wala rushwa na mafisadi lakini kazi ya pccb wakishamaliza file lote wanampelekea huyu bwana yeye ndo awafikishe mahakamani kwa hiyo mapambano ya ufisadi ktk tanzania hayatafanikiwa bila huyu bwana kua shupavu, yeye kila file analopelekewa anadai ushahidi haujitoshelezi kwa hiyo hawezi mburuza huyo mtuhumiwa mahakamani eti serikali inaweza shindwa kesi na kudaiwa fidia kubwa ambayo ikilipwa italeta hasara kwa serikali, swali la kujiuliza hadi pccb wampelekee file si kua wamejiridhisha kuna kesi ya huyo mtu kujibu kwani hata pccb wana kitengo cha sheria!