ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 643
- 1,603
Umoja ndiyo nyenzo muhimu ya kukabiliana na changamoto ambazo zinatukabili leo na kesho. Kama nchi ambayo imejaliwa utajiri na tofauti za kijamii mbalimbali kama vile utamaduni, kabila, dini, lugha, na siasa, tunahitaji kusimama pamoja ili kuweza kujenga taifa moja la Tanzania ambalo kila mmoja anafurahia kuwa sehemu yake.
Kwa hiyo mapambano na shida za kundi moja ni mapambano na shida zetu sote. Kwa kuzingatia historia yetu ya kupigania umoja na maelewano katika bara la Afrika na duniani kwa ujumla, ACT inatambua umuhimu wa umoja na ushirikiano na majirani zetu na hivyo itashirikiana na nchi nyingine katika kusukuma mbele ajenda ya Umoja wa Afrika ili kuweza kujenga nguvu za pamoja katika kujiendeleza kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa.
Kwa hiyo mapambano na shida za kundi moja ni mapambano na shida zetu sote. Kwa kuzingatia historia yetu ya kupigania umoja na maelewano katika bara la Afrika na duniani kwa ujumla, ACT inatambua umuhimu wa umoja na ushirikiano na majirani zetu na hivyo itashirikiana na nchi nyingine katika kusukuma mbele ajenda ya Umoja wa Afrika ili kuweza kujenga nguvu za pamoja katika kujiendeleza kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa.