ACACIA Mining PLC: We do not agree with President Magufuli Committee's findings...

Kumbuka "East African Mine" Wao walijenga mpaka Underground Train, wakavuna wakachoka wakajiondokea miaka hiyoooo. Sasa sisi tunavuna makapi "Tailings" na bado tunapata. Kimsingi yale madhahabu yaliyojaa huko Germany, Rome, etc ndo hizo za East African Mines.
Sasa basi huko Buzwagi na Kakora si Barric Gold Tanzania President miaka hii ya karibuni "Mr. Deo Mwanyika" wakuu wa Mgodi wa Buzwagi na Kakora wapo hapa nchini. Waitwe kwenye public wauleleze umma walikuwa wanasafirisha nini. Maana sasa tuna evidences. Wakikataa kusema ukweli walichokuwa wanapeleka nje. Basi tusubiri tarehe ikifika mbele ya uso wa Mungu. Naye watamdanganya?????
Please Mr. Mwanyika na timu yako njoo utoe mashaka hapa.

Mkuu umesema vizuri sana.

Ila ondoa mambo ya Mungu hapo.

Waletwe, waulizwe wotoe majibu mubashara tena hata kwa Damu kuwavuja ili wapate akili na ili iwe fundisho kwa wengine wawe wanasema ukweli.

Mungu kumshilikisha, halafu Mungu mwenyewe ni huyu wa wazungu koko na warabu wajitoa mhanga na magaidi, ambaye ukitenda dhambi unatumbu unasamehewa uovu wote haukumbukwi!
Therefore, to involve God in this matter; it's completely wrong and it will be to late.
 
Mkuu umesema vizuri sana.

Ila ondoa mambo ya Mungu hapo.

Waletwe, waulizwe wotoe majibu mubashara tena hata kwa Damu kuwavuja ili wapate akili na ili iwe fundisho kwa wengine wawe wanasema ukweli.

Mungu kumshilikisha, halafu Mungu mwenyewe ni huyu wa wazungu koko na warabu wajitoa mhanga na magaidi, ambaye ukitenda dhambi unatumbu unasamehewa uovu wote haukumbukwi!
Therefore, to involve God in this matter; it's completely wrong and it will be to late.
Mwanyika anaishi kama yuko peponiiii million 40 kwa mwezi achilia mbali benefits zingine kama transport, communication et al lazima usaliti nchi aisee noma sana
 
wanaoendeleza unafiki ni nyinyi na wabunge wenu wa NDIOOOOOO!!!! mbona POMBE... wapinzani waliposusia sheria ya madini na wakaaamua kutoka nnje ya bunge POMBE kama kweli alikuwa anauchungu wakati ule angeungana na wapinzani kutoka nnje lkn alichofanya ni na yeye kuwa mmoja wa washangiliaji/wazomeaji wabunge wa upinzani wakati wanatoka nnje. leo hii utaniambii nini ili nimuelewe SIZONJE kuwa kweli anauchungu na TANZANIA YETU?
HII KUKURUPUKA NAYO NI TATIZO KUBWA KWA UTAWALA HUU....
Tunafurahia sasa ukurupukaji wa serikale juu ya kuwabana wawekezaji wa madini hii ni furaha ya muda tu tusubirie machungu ya baadae kutokana maamuzi ya kukurupuka bila kufata ushauri nasaha anaopewa kila siku.
tatizo ni paleee.. anaposema ''UKINILETEA USHAURI NDO UNAHARIBU KABISAAA.. NAACHA NA SIFATI USHAURI. ME SIPANGIWI.. ME SISHAURIKI''

Kwa akili yako, Unafikili kuwa John kwa nyakati zile hakuogopa Kitwangalization, Mwakyembelization and recently , Napenization !!?
Pia, ukiwa nje ya mfumo wa chama na serikali ni rahisi kusema na kukataa mambo ila ukiwa ndani ni ngumu sana yaani ni sawa na kumsikiliza mshabiki wa mpira akisema piga hapa pasi, funga au mchezaji angecheza hivi.

Ila ngoma inakuwa ngumu siku uyo huyo mshangiliaji akipewa nafasi hiyo kucheza nasi nje tunaanza habari zake zilezile na aliyepewa nafasi hachezi chochote kile.

Kwa mfumo wa Tanzania na Katiba yetu hilo linawezekana tu mtu akiwa Rais ndiyo unaweza ukaongea au ukaamua upendavyo!

Mfano, cdm ilisema EL ni mchafu baadaye akaalikwa humo. Ni watu wangapi waliokuwa na nguvu na utu wa kuachia nafasi zao za kisiasa, kwa hiyo mifano elewa kuwa siasa ni ngumu na inaunafiki sana.

Na kuhusu wazee wa ndiyoooooo, naelewa ni janga.
Yaaaani, mimi hili Bunge letuni Sawa kabisa na "baby care centre" kazi yao ni kunywa chai ya maziwa ya NIDO na Nescafe, kujizungusha kwenye viti na mwisho kusinzia baadaye, wanazindukia kwenye "kibwagizo cha Ndiyoooooo"

Tanzania, "hilo linaloitwa bunge ndiyo wafanyakazi hewa namba moja"

Ila Kwa hili, JPM anastahili pongezi nyingi na kuungwa mkono nawatanzania wote wenye mapenzi mema na nchi yetu pasi kuangalia nani ni nani, vyama, dini, na vitu kama hivyo.
 
Mwanyika anaishi kama yuko peponiiii million 40 kwa mwezi achilia mbali benefits zingine kama transport, communication et al lazima usaliti nchi aisee noma sana

Ni kweli kabisa ulichokisema.
Hapo, hujasema waliokuwa wanasaini hii mikataba kwenye vungu za vitanda vyao!

Maana, nakumbuka BWM alichotufanyia ni majanga, mfano alikuja kufungua mgodi huo wa nyamongo akapewa zawadi ya buti imetengenezwa kwa dhahabu na bado mikataba ameisani uvunguni ni hatari sana.
Mfano, mwingine huyo BWM alikuwa anavaa mikufu ya dhahabu minene kweli wakati mmoja tulialikwa pale ufunguzi wa barabara ya mpaka wa Sirari na Isibania Kenya yaani Mr President ,alikuwa Kama Sonko huyu gavana wa hapo Kenya anavyovaa madini.

Madini yetu yamepotezwa na watu tuliowaamini.

Ngoja, Rais Magufuli naye ajaribu kuturudishia angalau nusu ya tulivyoibiwa na hawa wazungu koko kwa kusaidiwa na wazungu pori (waafrika wenzetu waliojifanya wazungu).
 
wewe unaupeo wa sisimizi

Mkuu, Mbatamo,
Huyo jamaa anayejiita "Nyanjomigire" atakuwa hajitambui kabisa.
Up stair yake ina-short au baadhi ya wire zimechomoka za kuunganisha na kutathimini mambo kama haya
 
Ukishinda na kulala njaa siku ya kwanza, ya pili, ya tatu na ya nne. Siku ya tano ukijiuliza kwa nini unalala njaa? Hapo akili yako imeanza kufanya kazi. Mnaohoji serikali ilikuwa wapi miaka yote, naona mnataka kuchanganya msiba na sherehe sehemu moja.
 
DOKEZO BAADA YA KUCHUNGULIA RIPOTI
  • Makontena yalikuwa hayawekewi seal (utepe wa usalama baada ya sempo kuchukuliwa) kwa sababu hiyo kulikuwa na mwanya wa mkaguliwa ACACIA kuongeza chochote anachotaka. seal ilikuwa inawekwa siku kadhaa baada ya kontena kutaka kusafirishwa.
  • Kokote duniani mkaguzi ndie anae nunua au kuagiza na kuweka seal baada tu ya kukagua, lakini katika hili kanuni hii ilikuwa haitumiki
  • Seal zote zilikuwa zinaagizwa na mkaguliwa(ACACIA) kinyume cha utaratibu wa uagizaji wa seal,kwa misingi kuwa mkaguzi lazima aagize seal kwa ajili ya usalama wa kulinda rekodi zake katika mali iliyokaguliwa zisibadilishwe..
  • ACACIA,SGS,TMAA wote kwa pamoja walikuwa wanaufahamu utaratibu huu muhimu, kwa nini waliukiuka?
  • Nani anajua endapo ACACIA alikuwa anaagiza seal zaidi ya moja zenye namba zinazofanana?
maswali ni mengi sana waheshimiwa labda tu cha msingi tukae pembeni tuangalie kinachojili, maana haiingii akilini eti TRA wawaruhusu wafanyabiashara kuwa na seal zao binafsi kwa ajili ya kufungia walichokikagua au TANESCO waturuhusu kila mtu aweke seal aliyonunua yeye kwenye mita ya umeme, hivi vitu vinaingia akilini kweli watanzania?
 
Nimesoma comments zenu na nina wastaajabu wengi munakurupuka kama Magufuli. Mukicheza mutapata hasara kweli kweli. Kuna mikataba na mikataba ni baina ya serikali ya CCM na makampuni ya nje. Na mikataba ipo tangu Mwalimu alipokuwa raisi. Turudi huko tuangalie mikataba utakuta kuwa Tanzania wana asili mia 30 katika mikataba chungu nzima. Mikataba ya Alamasi, tanzanite, dhahabu, makaa ya mawe, Uranium, GAS na OIl, n.k. Kuna awamu ya Nyerere, Mkapa, Mwinyi, Kikwete halafu Magu ndio aje afute?????.. Munacheza au nini?. Wote ni walaji hao na chama chao kimoja. Inachosikitisha ni kuwa RAISI ameyabeba kifuani wakati haya mambo yalikuwa yafuatiliwe kwa utaratibu wake mpaka yajulikane. Wengi katika chama ni wezi na kuwasafisha ni kazi kubwa. Kama ACACIA ni wezi kuna wenzake 39 watanzania wanao shirikiana nao. Hawezi muwekezaji kuja kuiba mali ya nchi bila mwenyeji wake.
 
Wazungu wamesema thamani ya huo mchanga ni 300m nyie mnasema 1tr si muwape hiyo hela mkauze, tatizo liko wapi?

Waliwachia mgodi wa Tulawaka tena wakawapa na mtaji mtwambie umasikini wa runzewe umeisha?
 
Hacha uoga. Kilichoko kwenye containers ni tofauti na kilichoandikwa. Period. hizo mbwembwe nyingine hazina tija. Pia containers zote hazina tag kuonyesha kilichomo ndani. Wenyewe ndo wamevunja mkataba.
says who?kamati iliyoundwa na upande mmoja wa mkataba?yani serikali katika hili imekuwa prosecutor,judge and executioner!!!!
 
Hawa wazungu ni wezi wakubwa toka Lin mzungu akasema ukweli na wakiwatumia vibaraka wa kiafrika. Juzi tu tulipata Uhuru kwa shida sasa na hawakupenda kuondoka LEO wanaisakama Afrika kidigital kwahiyo hawawezi kusema ukweli
 
Kumbe kwa akili yako ni vipi?
Hao wanasheria wenu walikuwa hawajui wanacho saini? Unajua maana ya kusaini au kuweka Dole Gumba? Ni kwamba ulikubaliana na hicho ulichosaini maana kabla ya kusaini ulipewa muda wa kupitia mikataba na kujiridhisha kuwa KILA KILICHO ANDIKWA NI SAHIHI!!
Unless unataka kuniambia hawa waliosaini hawajui lugha ya mikataba maana HAKUNA MKATABA ULIO ANDIKWA KWA KISUKUMA AU KIZINZA!!!Mikataba yote ni kwa kimombo lugha ambayo hata JPM bado inampa shida pamoja na udaktari wake!!!
Hongera sana .kwa hiyo ushauri wako themselves kibiwa?
 
Mitanzania mioga ya kulinda mali zao haifai kuishi katika nchi yetu. Tuachieni Rais wetu mzalendo alipiganie taifa
 
Haya makampuni ni majina tu. Mule ndani kama SGS kuna wabongo wenzetu wanafanya kazi. Tusitishane kwa majina ya makampuni.

Rushwa zipo tu hata Europe na USA. Ndio itakuwa Africa? Katika hili nipo na Mhe. Rais. Hata kama tutapoteza pesa thru fine na tupoteze tu ila message itakuwa imeshakuwa sent and delivered. Hapa kati walituchezea sana hawa majamaa.
 
Wazungu wamesema thamani ya huo mchanga ni 300m nyie mnasema 1tr si muwape hiyo hela mkauze, tatizo liko wapi?

Waliwachia mgodi wa Tulawaka tena wakawapa na mtaji mtwambie umasikini wa runzewe umeisha?
Kitu ambacho wengi tunakisahau ni kuwa Wazungu wanaweza tumia kivuli cha mchanga kusafirisha Madini/Gold concentrates. Labda mjiulize Tanzanite imafikaje Kenya had Kenya inakuwa nfldio the leading export wa Tanzanite?

Kuna report ya South Africa nao wanalia utoroshwaji wa dhahabu yao. So hata hapa huenda wanatumia kisingizio cha mchanga kutorosha Dhahabu.

Nimesoma utetez wao bado hauna hoja. Sisi tunaongelea viwango vya madini kwenye macontainer ya Bandarini, wao wanaongelea Historia.

Yani wanataka kuuaminisha umma kwa historia. Ingefaa sana kama wanatoa povu baada ya wao kupima viwango vya Madini kwenye mzigo wa bandarini.

Wana ongea Non sense. Mtu anatoa povu kutokea UK. Na watanzania bila kujiongeza, bila utafiti wanakurupuka na kuungana na wahuni. Ni wazungu hawa hawa wanaosema "without a research you don't have the right to speak". Sasa leo wao wamepata wap hiyo nguvu ya kutokwa povu bila kufanya utafiti kwa kutumia sampuli za mchanga wa kwenye containers zilizopo bandarini?

Hapa hatuongelei historia, t unaongelea viwango vya Madini kwenye Yale macontainer ya bandarini.
 
Back
Top Bottom