Huku viongozi wazalendo na makini wakiwa wanapungua siku hadi siku katika chati za uongozi wetu wa kitaifa inatia moyo pale tunapoona viongozi vijana wakiwa mstari wa mbele kutetea maslahi ya taifa katika nafasi zao mbali mbali.
Katika bunge la Afrika Mashariki, mbunge wetu Abdallah Mwinyi, amekua mstari wa mbele katika kutetea maslahi yetu ya taifa ukijumlisha michango yake ya mara kwa mara ndani ya bunge hilo (ambapo wabunge wetu wengine wamekua siyo wachangiaji wazuri).
Kutoka kutetea kasi yetu ya kujiunga na soko la pamoja ndani ya bunge hilo ambapo nchi za jirani haswa Kenya na Rwanda walikua wanatukaba shingo kufungua mipaka yetu kwa bidhaa zao, hadi kutetea ongezeko la vibali vya kazi kwa wafanyakazi wageni nchini na kusema kua vibali hivyo ni kwa wafanyakazi wote wakiwemo wa nchi wanachama wa EAC huku akijibu kwa umakini mzuri lawama za wabunge wa nchi hizo jirani ni mfano mzuri wa umakini wa huyu mheshimiwa.
Ni vizuri tuanzishe utamaduni wa kuwapa pongezi viongozi wetu wachache wa kitaifa wanaposimamia kazi zao kwa umakini na uzalendo. Pongezi kwa kazi nzuri Mh. Mwinyi, tunategemea kuona mchango wako zaidi katika uongozi wa taifa letu miaka ijayo baada ya kumalizia muda wako EALA hapo 2017.
Mharakati
Katika bunge la Afrika Mashariki, mbunge wetu Abdallah Mwinyi, amekua mstari wa mbele katika kutetea maslahi yetu ya taifa ukijumlisha michango yake ya mara kwa mara ndani ya bunge hilo (ambapo wabunge wetu wengine wamekua siyo wachangiaji wazuri).
Kutoka kutetea kasi yetu ya kujiunga na soko la pamoja ndani ya bunge hilo ambapo nchi za jirani haswa Kenya na Rwanda walikua wanatukaba shingo kufungua mipaka yetu kwa bidhaa zao, hadi kutetea ongezeko la vibali vya kazi kwa wafanyakazi wageni nchini na kusema kua vibali hivyo ni kwa wafanyakazi wote wakiwemo wa nchi wanachama wa EAC huku akijibu kwa umakini mzuri lawama za wabunge wa nchi hizo jirani ni mfano mzuri wa umakini wa huyu mheshimiwa.
Ni vizuri tuanzishe utamaduni wa kuwapa pongezi viongozi wetu wachache wa kitaifa wanaposimamia kazi zao kwa umakini na uzalendo. Pongezi kwa kazi nzuri Mh. Mwinyi, tunategemea kuona mchango wako zaidi katika uongozi wa taifa letu miaka ijayo baada ya kumalizia muda wako EALA hapo 2017.
Mharakati