Ni maduka ya kimataifa. Hata Tanzania yanaweza kuanzishwa.
Ni maduka yasiyofungwa iwe mchana iwe usiku, iwe jumapili iwe sikukuu. Yako wazi 24/7
Yanaitwa Seven Eleven kwa sababu mwanzoni maduka ya Seven Eleven yalikuwa yakifunguliwa saa moja asubuhi mpaka saa tano usiku.
Wazo la kutofunga maduka ya Seven Eleven lilikuja baada ya gemu ya mpira. Wateja walikuwa wengi sana usiku wa siku hiyo.
Ni maduka yanayopatikana karibu na makazi ya watu. Kwa wenzetu hakuna maduka ya rejareja mitaani (kwa mangi)
Ni maduka yanaouza bidhaa za aina nyingi sana ikiwemo chakula, vitafunio, dawa za miswaki, dawa, sabuni, sigara, mpaka oil za magari.
Polisi hawachezi mbali na maduka haya kwa sababu maduka yake yana historia ya kuvamiwa na majambazi. Kwa upande mwingine ni heri kwa sababu polisi wanakuwa karibu na nyumba za watu wakati wa usiku.
Maduka ya Seven Eleven hutoa ajira hasa kwa wanaotafuta kazi ya pili.
Ni maduka yanayotambulika kiserikali hivyo ukusanyaji wake wa kodi ni wa uhakika.
Ni maduka yanayochangamsha miji. Sio Bongo muuza chipsi wa mwisho akifunga kibanda chake saa tano na nusu usiku mji mzima umezima.
