4G ya halotel ni feki au ndiyo H+?

4G ya halotel ni feki au ndiyo H+?

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,185
Reaction score
24,574
Kuna mambo yanashangaza sana 3G ya halotel ina kasi na nguvu kuliko 4G ya halotel hili linafikirisha sana

Ukitaka kuamini weka 3G ya halotel upime speed ikisha uweke 4G ya halotel upime speed...Majibu yake yatakushangaza kuwa 3G ya halotel ni bora ina kasi kuliko 4G ya halotel

4G ya halotel ni mchongo, na huenda ni feki kabisa wala sio 4G halisi kama wanavyotuongopea nchi zetu hizi tunadanganywa sana eti halotel wana 4G?[emoji23]
 
Ni kweli kabisa mkuu.Jamaa yangu leo hii asubuhi alikuwa analalamika network yake kusoma E zaidi ya saa 3 na aliweka 4G baada ya kubadilisha 3G mtandao ukakaa sawa.
 
Ni kweli kabisa mkuu.Jamaa yangu leo hii asubuhi alikuwa analalamika network yake kusoma E zaidi ya saa 3 na aliweka 4G baada ya kubadilisha 3G mtandao ukakaa sawa.
Kabisa
 
Natumia Halotel. Sijui kwann sihami ila ni mtandao wa kiwaki kingese.
 
Ni kwel kabisa.. yaan 4G ilitakiwa ukitouch link isiload ifunguke kama unavyofungua apps kwenye cm.. lakin et ina load weeeee..
Hizi 4G ni mchongo tu download speed haizid MB 1 khaah
 
Mimi huwa line inazima na kuandika viettel sifanyi mawasiliano yoyote hata siku mbili baadae inarud mtandao wa kipumbavu sana huu
 
Mimi sijaona 4g mwanzoni walipotangaza ndio ilikuwepo Sasa ivi 3g ndio Ina nguvu tigo na voda na Airtel ndio majanga

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kuna mambo yanashangaza sana 3G ya halotel ina kasi na nguvu kuliko 4G ya halotel hili linafikirisha sana

Ukitaka kuamini weka 3G ya halotel upime speed ikisha uweke 4G ya halotel upime speed...Majibu yake yatakushangaza kuwa 3G ya halotel ni bora ina kasi kuliko 4G ya halotel

4G ya halotel ni mchongo, na huenda ni feki kabisa wala sio 4G halisi kama wanavyotuongopea nchi zetu hizi tunadanganywa sana eti halotel wana 4G?[emoji23]
Nafikiri sababu ni uwepo wa 4G kwenye eneo ulilopo. Yaani kama mnara uliopo hauna uwezo wa 4G basi ukiweka 4G hutapata internet vizuri au kabisa kwa kuwa unachokiomba hakipo katika mnara huo, lakini ukaweka 3G kwa kuwa mnara umefungwa kusapoti hiyo 3G tu basi utafanya kazi vizuri.

Ni kama leo mtu akiweka 5G halafu akakaka kijijini kabisa ambako minara haijawezeshwa, simu yake haitapata internet kabisa, isipokuwa akiweka ichague yenyewe automatically, itachagua ule mtandao unaopatikana na atapata internet kwa 3G au 4G.

Huo ndio uelewa wangu, ila kwa msaada na ufafanuzi ulionyooka, Mkuu Chief-Mkwawa na wengine watatusaidia zaidi.
 
Mi Halotel mwenyewe nimeivumilia kinyama yaani ado apo mwanzoni mwa mwaka huu nilipoamua kuachana nayo rasmi
 
Back
Top Bottom