32 bit vs 64 bit

Then sitaweza kukujibu kitaalamu ukanielewa..Thanks

Hehehe mkuu una biti, hutomjibu akuelewe kwa sababu ipi hasa? Kujua qword na dword hakumsaidii mtu kuelewa computer architecture, a word is simply 2bytes, dword ni 4bytes na qword ni 8bytes, ni unit tu ya bits of information sawa na unit nyingine, ungetumia neno 4bytes ungeeleweka vizuri tu.

CHIEF MKWAWA sioni alipokosea, ni kweli 32bits processors zina~max at 4GB na 64-bits zinaenda hadi 16.8 million terabytes.
Sababu ni simple tu, sioni kwa nini unazunguka around the bush.

Processor inavokua inataka kuexecute instruction flani inayoinvolve kuweka au kufetch data kutoka kwenye memory inatumia address, hii address ndio point ambayo hiyo data inapatikana kwenye memory, address zenyewe zinakua in bits, mfano 32-bit processor ina address ambayo ni 32-bit, 32-bits maana yake kuna uwezekano wa 2^32 different combinations za address ambayo ni approximately 4Billion bits = 4GB. Sasa ukiwa na RAM zaidi ya 4GB kwenye 32-bit processor haina maana kwa kua processor yako ikiomba data itakua inaomba data ambazo zinapatikana ndani ya 4GB peke yake, hizo sehemu nyingine zote hazitumiki.

Mbona very easy kuelezea mkuu
 
nkwarisambu ndio nawaza michezo we inakuuma nini mimi nikiwa nawaza kucheza michezo
je mimi ninaewaza michezo na anaewaza kuzini nani bora mind your words kijana usinichukulie poa
 
Nimepata somo kwa kweli nahisi mie pia ni muhanga wa 32bits maana hata video nikiweka kuna ambazo inacheza slow motion na zingine video ila zinacheza audio......au kunashida nyingine wakuu???? Nawasilisha tafadhali
 
Nimepata somo kwa kweli nahisi mie pia ni muhanga wa 32bits maana hata video nikiweka kuna ambazo inacheza slow motion na zingine video ila zinacheza audio......au kunashida nyingine wakuu???? Nawasilisha tafadhali
• Inawezekana kuna programs nyingi zinazorun kwenye background na pc yako inakuwa inashindwa kuperform kwa ufanisi video playback, kutokana na pc yako kuwa na uwezo wa kawaida lakini bado ukawa unatumia programs nyingi at the same time.
• Inawezekana ukawa hukufanya installation ya drivers za graphics card za pc yako. Bila graphics card drivers kuwa installed kwenye pc yako, windows inashindwa kutambua uwezo wa video ram kenye pc yako na pia aina ya grahics card iliyo kwenye pc yako. Hivyo inakuwa ina-approximate kuwa una 256MB ambayo ni ndogo sana kwa sasa hivi na haiwezi kutumika kwa kila app kwenye pc. Hivyo make sure umefanya installation ya grahics card driver.
 
Mkuu umeeleza vzuri na nimekupa like yangu....ila Mkuu unavosema kuna computer ambazo ni 32bits Na nyingine ni 64 bits nadhani unakosea kidogo...kwa uelewa wako wa computer nadhani ungesema OS ndo inaweza kuwa 32 bits au 64 bits..
Hata mimi nakuunga mkono OS is what matters
 
Thanx worrior, I tried the options given but kila nilipojaribu kuinstall iliniambia kua my computure doesn't meet the minimum requirements,nika update software but still the problem persists.
Help please
 
Yeah nakumbuka pindi tunajifunza programming (c) kwene kozi ya CS50,Prof. Malan alisema the same thing.
 
Msaada jinsi ya kuibadili 32 kwenda 64 bit
angalia kama hardware yako inakubali 64bit kama haikubali huwezi badili hadi ununue hardware mpya na kama inakubali itabidi ufanye clean isntallation ya software ya 64bit.
 
angalia kama hardware yako inakubali 64bit kama haikubali huwezi badili hadi ununue hardware mpya na kama inakubali itabidi ufanye clean isntallation ya software ya 64bit.
Shukrani Chief naangalia vipi ili kujua kama inakubali 64 bit au la?
 
Tatizo hapa naona mmeamua kumvuruga mtoa mada, hey dogo sikia hapa unazungumzia mtiririko wa Bomba la maji ya kipenyo cha 1.5 na 3ml kiwango cha maji kinachopita lazima kiwe tofauti, aidha katika mifumo ya kompyuta kuna kitu kinaitwa compatibility hivyo hiyo gemu unayoizungumzia specififications zake haziko compatible na 32bit bali 64bit.

Nyongeza kama utataka
Mfumo wa usafirishaji wa DATA kwenye compyuta unatumia hesabu za Binary yaani hesabu zako zote lazima u multiply kwa mbili, miaka ya 2000 kulikua na Window 97 second edition ambayo ilikua iko compatible na 16bit na kabla ya hapo tulikua na 8bit.

Pole kama nitakua nimekuvuruga zaidi na tatizo litakua kwako zaidi kuliko kuwa kwetu
 
Sijaelewa vizur swali mkuu ila
pc natumia dell latitude window 7 professional

Core i3-2310M 2.10 Ghz
RAM 4GB
32-bit os
hio inakubali 64bit.

itabidi ufanye clean install.

tafita cd ya windows 64bit kisha install windows kwa kuformat local disk c
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…