2015 ni CCM au CHADEMA: Nini matarajio yako?

2015 ni CCM au CHADEMA: Nini matarajio yako?

MJENGA

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
883
Reaction score
852
Bila ubishi watanzania wengi wameichoka CCM. Wapo wenye sababu ya kuichoka kwa kusema kuwa ni chama kikongwe hivyo wanataka chama kipya chenye mawazo mapya. Wapo pia wenye sababu ya kwamba CCM ni chama chenye kashfa nyingi za ufisadi na mengine mengi. Ndani ya kashfa hizo wapo wanaozielewa kwa upana wake lkn pia wapo waliolishwa vichwani mwao na hao wanafuata tu upepo. Lakini wapo wanaosubiri maamzi ya wengi ndiyo wabadili maamzi yao.

Wapo wasiopenda kuiondoa CCM madarakani kwanza kwasababu ya historia ya amani na utulivu ambayo misingi yake imejengwa na CCM. Kundi hili linaona kuwa kuiondoa ccm madarakani ni kukaribisha serikali ya kihuni ambayo haitazingatia misingi ya amani bali uholela na vurugu.

Kundi hili kubwa ni la wazee na akina mama ambao aghalabu wameshuhudia mapito mbali mbali ya taifa na changamoto ambazo hawataki kuziona Zikijirudia. Hili ni kundi lisilowaamini wapinzani. Linawaona kama watu wenye nia mbaya na taifa na kwamba si bure wanatumika na watu wa nje kuvuruga nchi.

Yote kwa yote, iwe CCM ama CHADEMA watanzania lazima tujiulize kwamba tunapofanya maamuzi 2015, tunayafanya tukiwa ktk hali ya jazba ama chuki, ama kwa kutumia hekima na busara?. Huenda kila mtu ana maslahi na chama atakachokichagua lkn je chama hicho kina utaifa ndani yake? Ni lazima tujiulize. Uchaguzi 2015 hauhitaji jazba wala hasira. Tuamue kwa kuzingatia umoja wetu, amani yetu, utaifa wetu na wala si kwa msukumo wa dini, kabila, wala rangi.

Maamuzi yetu yasibebwe na matarajio makubwa ili kuepusha nchi kumwaga damu katikati ya safari ya serikali itakayochaguliwa. Yapo mambo yatakayowezekana kufanyika lkn tusitembee na vivuli vya yelusalemu takatifu vichwani mwetu. Tusipoiona tutachinjana. Tuwapime wanasiasa kwa kauli, matendo na udhati wa dhamira zao katika kulitumikia taifa. Tuzibaini na kuzitambua ngozi za mbwamwitu kwenye miili ya kondoo ili tusijutie baadae.

Mimi na wewe na yule tujiulize kama ni CCM itatufanyia nini na kama ni CHADEMA itatufanyia nini?. Tuongozwe na utashi wa kiroho ktk kuamua badala ya jazba na chuki. Tukiamua kwa hisia itatugharimu na iko siku thread hii itarejeshwa jamvini na kugombaniwa na wanajamvi kama njugu.

NI UNABII TU!!!.
 
Communist UNIP ya Zambia ilifanyaje?
 
CDM haiwezi kupewa nchi kwa sasa ila endeleeni kujitahidi tutawafikilia 2035!
 
Bila ubishi watanzania wengi wameichoka ccm. Wapo wenye sababu ya kuichoka kwa kusema kuwa ni chama kikongwe hivyo wanataka chama kipya chenye mawazo mapya. Wapo pia wenye sababu ya kwamba ccm ni chama chenye kashfa nyingi za ufisadi na mengine mengi. Ndani ya kashfa hizo wapo wanaozielewa kwa upana wake lkn pia wapo waliolishwa vichwani mwao na hao wanafuata tu upepo. Lakini wapo wanaosubiri maamzi ya wengi ndiyo wabadili maamzi yao.

Wapo wasiopenda kuiondoa ccm madarakani kwanza kwasababu ya historia ya amani na utulivu ambayo misingi yake imejengwa na ccm. Kundi hili linaona kuwa kuiondoa ccm madarakani ni kukaribisha serikali ya kihuni ambayo haitazingatia misingi ya amani bali uholela na vurugu. Kundi hili kubwa ni la wazee na akina mama ambao aghalabu wameshuhudia mapito mbali mbali ya taifa na changamoto ambazo hawataki kuziona Zikijirudia. Hili ni kundi lisilowaamini wapinzani. Linawaona kama watu wenye nia mbaya na taifa na kwamba si bure wanatumika na watu wa nje kuvuruga nchi.

Yote kwa yote, iwe ccm ama chadema watanzania lazima tujiulize kwamba tunapofanya maamuzi 2015, tunayafanya tukiwa ktk hali ya jazba ama chuki, ama kwa kutumia hekima na busara?. Huenda kila mtu ana maslahi na chama atakachokichagua lkn je chama hicho kina utaifa ndani yake? Ni lazima tujiulize. Uchaguzi 2015 hauhitaji jazba wala hasira. Tuamue kwa kuzingatia umoja wetu, amani yetu, utaifa wetu na wala si kwa msukumo wa dini, kabila, wala rangi.

Maamuzi yetu yasibebwe na matarajio makubwa ili kuepusha nchi kumwaga damu katikati ya safari ya serikali itakayochaguliwa. Yapo mambo yatakayowezekana kufanyika lkn tusitembee na vivuli vya yelusalemu takatifu vichwani mwetu. Tusipoiona tutachinjana. Tuwapime wanasiasa kwa kauli, matendo na udhati wa dhamira zao katika kulitumikia taifa. Tuzibaini na kuzitambua ngozi za mbwamwitu kwenye miili ya kondoo ili tusijutie baadae.

Mimi na wewe na yule tujiulize kama ni ccm itatufanyia nini na kama ni chadema itatufanyia nini?. Tuongozwe na utashi wa kiroho ktk kuamua badala ya jazba na chuki. Tukiamua kwa hisia itatugharimu na iko siku thread hii itarejeshwa jamvini na kugombaniwa na wanajamvi kama njugu.




NI UNABII TU!!!.

matarajio yangu na ya watanzania walio weng ni kuona mabadiliko ya kwel na mazuri ktk nyanja zote za maisha ya mtanzania.tanzania ni nchi tajiri kwa maliasili ivo tunaitaji chama makin kinachoweza kutuvusha toka hapa tulpopokwama mpaka kwenye mafanikio haris.tumekwama kwa muda wa miaka 50,maendeleo tuliopata hayaendani na raslimali tulizonazo.ccm imetukwamisha,ni adui wa maendeleo ya watz.chadema ni mbadala wa ccm.
 
tatizo kubwa bado watanzania wengi hasa walioko vijijini wanaamini ccm ni chama kilicho wazaa, lkn hakika tukiendelea na mtazamo huu maendeleo tz ni kichwa cha mwenda wazimu.
 
Asanteni wanajamvi kwa maoni yenu. Lakini point yangu ya msingi hapa ni kutaka kujua position ya watz ktk kuamua kwa busara. 2015 tunaweza kuamua kwa hasira halafu tukalamba dume. Ushauri wangu ni kuwa tuwe makini kwani shetani hupenyeza rupia penye udhia. Ni mtazamo tu!
 
Back
Top Bottom