Hiii yote imesababishwa na Mkuu wa nchi sababu kauli alizozitoa yeye na chama wakati wa kuapishwa sasa ndio zinajionesha wazi kwamba walitengeneza jamii ambayo imeingiwa na chuki amabayo italipeleka taifa kubaya
Hii ndio Tanzania yetu.....imeoza kwa uongozi mbovu kupita kiasi.....halafu mtu bado anasafiri nje kwa kisingizio cha "STATE VISIT" jamani hatuna viongozi...hivi huko Kenya kulipokuwa na matatizo ulimuona kiongozi akisafiri?! Zaidi walikaa pamoja kujadili cha kufanya "KWELI BABA WA TAIFA ALIONA...
Tatizo lako wewe litakuwa kama la wale waandishi wa habari walioripoti kuwa yule mwenzao amepigwa na mtu aliyekuwa na hasira nae na wala si serikali.....na kisha wakajaza juu ya vichwa vya habari.....SABABU BADO HUJAJITAMBUA na ndio maana unatetea utumbo tena kwa mifano....
Labda si Tanzania niijuayo mimi kwani wangapi wamefungwa toka wakutwe na makosa?!?labda mimi na wewe ambao hatuna hata BIBI na BABU waliowahi kuwa na cheo katika nchi hii.....ila kinachohitajika ni kwamba sisi wenyewe watanzania tubadilike na kuamua kujikomboa na jinamizi hili...
Ninachoweza kasema ni kwamba viongozi wetu wa tanzania bado hawajajitambua kuwa wao ni viongozi wa nchi yenye mahitaji ya maendeleo kwaniyo wao kazi Yao ni kukurupuka tu na mambo ili waojioneshe kwa watawaliwa wao kuwa wanafanya kazi.......masikini Tanzania yangu......
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.