Mzee aliyeingilia Kati suala.la Askari barabarani na akasikilizwa tunaomba aingilie Kati pia suala la tozo, asikae kimya maana ni moja wapo ya njia ya kutetea wananchi
Wakuu nashukuru nilipata mzigo wangu na kwa bahati nzuri sikukatwa kodi isipokuwa nilitozwa gharama za posta kiasi cha tsh 2350,asanteni sana kwa ushauri ambao nadhani next time nitafanya mazungumzo na seller kabla ya kununua mzigo ili nijue invoice itakavyokuwa baada ya kununua mzigo
Wakuu status ya mzigo wangu inaonyesha umezuiwa na Watu wa TRA ,uliingia toka 24/12/2019, Jana ndio update ikaonyesha" Held by customs" . Je watanijulisha kiasi cha kodi au mpaka nifuatilie? Na km kufuatilia nafuatilia posta au TRA? Plse wanaofahamu utaratibu
Mkuu kwani dispute haina muda maalum? Isije kuwa Jamaa wanakupotezea muda ili muda wa dispute uishe. Any way ,hao akina yanwen ,Malaysia post,nk wengine hata tracking number zao sio international ukienda POSTA wanakwambia hizo namba hazipo
Mimi nilshawahi Agiza mzigo ukasafirishwa na huyo agent lkn update ya Mwisho ni may 16 mzigo ulikuwa posted to counter south Africa, mpaka Leo haujafika tanzania, nilishafungua dispute na nilisharudishiwa fedha zangu, shipper mwingine wa hovyo ni Malaysia post
Ukishapata hiyo tracking namba km alivyokuelekeza Mdau hapo juu, download application inaitwa "Track24" au "17 track" zitakusaidia kutrack mzigo wako any time unapotaka
Ulizia hapo posts ulipochukua parcel inawezekana wamesahau hiyo ya Pili,Mimi ilitokea hivyo wiki moja iliyopita,kumbe yule anayechapisha vile vikaratasi vya kupokelea mzigo alisahau ikabidi akichape muda huo huo na nikapewa mzigo wangu,na ilikuwa posta ya mkoani
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.