Wadau,
Kwa hali hii, natamani vikao vya Bunge vianze kesho!!!! Hili ndilo Bunge la mseto wa ukweli. mweee.. Vijana, Wakulima, Wachungaji, Wanawake, Wafanyibiashara, Wazee, Wanaume, Wanamuziki, Wanataaluma, Mafisadi, Waganga wa kienyeji, Waadilifu... yaani ni fulu mixi. Asalaaale...
pamoja na yote haya lakini kuna wenye macho lakini hawaoni, kuna wenye masikio lakini hawasikii.sijui tuwasaidieje hawa na kwa uhakika kabisa ndio wanaoturudisha nyuma. Hatutachoka kuwahubiria na iko siku watafungua macho na masikio waweze kutumia kura yao kwa manufaa bora ya taifa letu.
Hebu jamani tufikiri japo kidogo tu,
hizi shule bila ya walimu, bila ya maabara, bila ya vitendea kazi kuna elimu kweli hapo? Hao walimu wachache wenyewe ndio wale wa voda faster hawana skills za kutosha za kufundisha na kimaadili ya ualimu pia nina mashaka nao. Hawa ndio tuwape watoto...
Hebu tuzungumzie japo kidogo tu kuhusu hali ya raisi wetu.
Mwaka 2005 alianguka pale jangani tukapewa sababu hizi na zile.
Ameenda Mwanza CCM Kirumba ameanguka tena jukwaani, sababu hazikosekani.
Mwaka huu wa uchaguzi tena ameanguka palepale jangwani hawachoki kutudanganya. Niliwahi kusoma...
hivi kweli kuna kitu gani cha kuwafagilia ccm?
Labda tuseme kwamba ni mabingwa wa usanii kwa ahadi zisizotimizwa, mafisadi number moja, mabingwa wa siasa za kuchafuana, mabingwa wa kula rushwa, heko kwa ubadhilifu wa mali za uma, aisee wanaweza kushinda kwa hayo. Kila ukimmulika ccm amechafuka...
Wengine sijui huwa wanafikiria vipi. Mi nafikiri fikra zao zimefika mwisho. Hawajui kuwa kuna zaidi ya hapo walipo sasa. Tufungue akili zetu, hakuna ambacho hakiwezekani endapo tuna nia ya kutenda kwa dhati.
sio kukurupuka kijana.
Huyu mmarekani anakuambia unapata misaada mingi kuliko nchi nyingi za afrika. Unarasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za afrika. Na bado huendelei,ameacha tu kukuambia kuwa wewe ni mpumbavu. Maneno haya yana maana hasa kama utakuwa unatafakari. Anamaanisha hawa viongozi...
Unajua ukweli ni kwamba,
"tusipojichunguza kwa nini hatuendelei wakati tunapata misaada mingi (kitu ambacho sipendi) na tuna rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za afrika hatutakaa tuendelee daima".
Kikwete atatuachia nchi katika mikono ya wahisani, sera zake hovyo, kauli mbiu usanii...
Tusipojichunguza kwa nini hatuendelei wakati tunapata misaada mingi (kitu ambacho sipendi) na tuna rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za africa hatutakaa tuendelee daima.
Serikali ya sasa inatuachia nchi katika mikono ya wahisani. Ni vipi tutegemee misaada??? Tunaposema kilimo kwanza ni...
Hapa sasa nakumbuka statement ya balozi wa marekani hapa nchini aliposema "tanzania isipojichunguza kwa nini haiendelei wakati inapata misaada mingi na ina rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za afrika haitakaa iendelee daima". Akutukanaye hakuchagulii tusi.kwa mtu mwenye akili na busara hili...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.