Ungekuwa na NGO yako basi isiyo uchwara, matusi haitusaidii na propaganda zenu. Tutadai hai zetu hadi mwisho. Kama wanamaslahi yao kwa Mwarabu wa Dubai wakawape ardhi kwao siyo kwetu.
Mashirika ya hiari yanayojishughulisha na kutetea haki za ardhi na haki za binadamu nchini tanzania asubuhi hii imetoa tamko la kupinga ardhi wa vijiji vya loliondo kutolewa kwa mwekezaji mmiliki wa kampuni ya obc anayefanya biashara ya uwindaji wanyama pori katika ardhi ya vijiji vya loliondo.
Sijui kama unaweza kudhibitisha hivyo visima. Wanaonyang'anywa ardhi wamasai si loliondo mjini. Hata kama kwa mfano kisima ikijengwa loliondo mjini, umeme ukawekwa wamasai wananufaika vipi? Wamasai wafugaji km kweli mwarabu anawajali anaowanyang'anya ardhi kwa nini hakuwai kuchimba bwawa la...
Kadi ya uanachama huandikwa jina la mtu, hata ikirudishwa haitafaa kutumia kumwandikia mtu mwingine. Sielewi dhana ya kurudisha kadi kama kweli ndo ushahidi na kielelezo cha kukihama chama. Kwa kauli ya Nape, hata wale wanaotoa ktk mikutano ya siasa, CDM, CUF na mengine huwa yanarudishwa CCM? Na...
Naona kila sababu ya kufutwa kwa cheo cha DC. Kumbe huwa ni ma kada wa chama na si watendaji wa Umma? Kweli tusikosee katika katiba mpya nafasi hii ifutwe. Tunataka watendaji wa serikali wanaowajibika kwa umma na si kwa chama, na chama chenyewe hii iliyogeuka maadui wa raslimali za nchi yetu...
Ukweli ni kwamba Dr. Slaa si mwanachama wa CCM tena kwa mjibu wa katiba ya CCM kwamba mtu akishakuwa mwanachama wa chama kingine uanachama wake ndani ya CCM unakoma mara moja. Tujiulize maswali ya msingi. Je Dr. Slaa ni mwanachama wa CDM? Kwa ndiyo hayupo tena CCM? Pili kwa nini Nape wa Ccm ndo...
Naunga mkono haya usemayo. Nafahamu familia nyingi huku simanjiro ambazo angali wazazi wao ni makada wa zuri wa CCM, watoto wao wamejitokeza waziwazi kuunga mkono M4C. Nakubaliana nawe kuwa kama watoto wa vigogo wa CCM hawatakuwa wa nafiki kwa chama cha wazazi wao, wapo wengi wanamezea mate M4C...
Kipindi kizuri na maswali mazuri yameulizwa, mbona sasa hatuoni majibu hapa? Tafadhali mwendesha kipindi utupe brief ya majibu ya maswali yaliojibiwa na hao walioulizwa.
Habari Tbc, kweli Daudi amefariki. Mazingira yameelezwa kuwa wakati polisi walipo vamia mkutano wa CDM ambapo wananchi ndo walikusanyika walipo mwona Dr. Slaa. CDM walikuwa wakijenga chama ngazi za vijiji na kata kwa kuongea na viongozi wa ngazi hizo. Daudi alikuwa ktk eneo hilo kuchukua habari...
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAARIFA HII INATOLEWA NA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUELEZEA MSIMAMO WAO KATIKA KAMPENI INAYOENDESHWA NA MTANZAO WA AVAAZ KUHUSU KUTAKA SERIKALI KUSIMAMISHA MCHAKATO WOWOTE WA KUUZA ENEO LA LOLIONDO KATIKA MFUMO WA IKOLOJIA YA SERENGETI UPANDE WA MASHARIKI...
Tungeungana tu watanzania wote nchini kuwaondoa wawekezaji wasio na tija kwa taifa letu. Si rahisi kwa walio madarakani kufahamu hilo ila sisi waathirika tunatambua ukweli huo. Go OBC go..............
Hata mimi nimesikia, kakuongeza hapo, ... Eti ni wapinzani wenye uchu wa madaraka... Binafsi sijawasikia wapinzani wakitoa matamko kuhusu huo mgogoro na malawi au labda JK anazungumzi wapizani wake kisiasa ndani ya chama chake anacho kiongoza. Mimi nimesikia na kusoma katika magazeti kauli za...
Mtazamo wangu kuhusu hilo la Tanganyika kuuawa kinyemela ni kuwa, Aliyekuwa anataka muungano ni Mwl. Nyerere na ili wazanzibar wakubali ikabidi akubali kupoteza taifa lake alilolipigania hadi uhuru.
Hapa ndipo usaliti wa Watanganyika ulipo. Sasa kwakuwa TANU iliwasaliti watanganyika na kuamua...
Shirika kama Nssf inajenga nyumba Arusha je wananchi ambao watakua wameacha/wameachishwa kazi kwa mazingira yeyote na ambao sasa hawaruhusiwi kuchukua mafao yao mpaka miaka 55 au 60 watakuwa na shares katika hizo nyumba maana bila shaka pesa zao ndizo zinazo tumika ktk huo ujenzi?
Migomo sasa inaanza kuzooleka masikioni mwa wananchi wa Tanzania. Jambo ambalo nadhani lapaswa kuangaliwa ni kwanini kuna migomo, Mfano madaktari wadai kugoma, TUCTA, walimu n.k. na maandamano ya wazee wa Afrika mashariki na wanafunzi vyuo vikuu. Najiuliza hivi watawala wanayaona haya? Kama...
Mgomo sasa inaanza kuzooleka masikioni mwa wananchi wa Tanzania. Jambo ambalo nadhani lapaswa kuangaliwa ni kwanini kuna migomo, Mfano madaktari wadai kugoma, TUCTA, walimu n.k. na maandamano ya wazee wa Afrika mashariki na wanafunzi vyuo vikuu. Najiuliza hivi watawala wanayaona haya? Kama ndiyo...
ndugu kadakabikile, huwezi kuwalaumu madaktari kwa kutogoma hapo hawali, kumbuka kila jambo na wakati wake, km wewe usingeweza kuamrisha uzaliwe ulaya, hata mgomo haukuwezekana hivyohivyo, wakati wake haukufika. Serikali inafahamu mapungufu yaliyopo ktk hospitali zetu ndo maana wao wanaenda kwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.