Nakubaliana nawe kabisa utapeli umezidi. Wiki mbili zilizopita nilipokea sms ikiniambia kuwa nimeshinda milioni kumi kwenye mtandao wangu wa vodacom. Nikapewa na namba ambayo niwasiliane na hao wahusika ili tuitwe kwenye ITV then tupewe pesa zetu kwani tuko kama watu 5. Lakini cha kushangaza...
Sasa usubiri wakianza kulipa wastaafu ndiyo utaudhika mpaka basi. Na ndiyo maana wazee wetu wakija chukua vihela vyao na wezi wako nyuma yao maana wanakuwa wamechoka mwanzo wa saa 12 asubuhi wako kwenye foleni mpaka network ya kichwa na halmashauri yote inachoka kufanya kazi, wanarudi hoi na...
Bravo Mkuu wangu, hawa wanataka kutulengesha hapa sasa iwe kila mtu akitaka kumwanika na kumchafulia mtu alete ishu yake hapa nooo hapa si pake ziko sehemu za kupeleka production kama hiyo na wenyewe wenye kazi yao watafurahi sana.
Kabisa ni majungu ya kutaka kumchafua na kwa vile ni karibu na uchaguzi basi imekuwa ni hadithi za alfulelaulela tu. Waje na proof hapo tutaona ni kweli lakini siyo kuleta za kuleta hapa. Ila wenye kazi zao na wanuse huko kama wanaweza kupata chochote. Kwangu mimi haiingii akilini asilani...
Msibishe ndugu zangu anachosema Pididy ni sahihi kabisaaaa. watoto hawa shauri ya tamaa wamekuwa hatari. Na hao wateja sasa kama wangekuwa hawaonekani ingekuwa sawa lakini pande zote mbili zinaona sawa hivyo inakuwa ngumu sana kudhibiti. Wateja msiende soko litakuwa hakuna!!!!!!!!!!
Ndugu yangu, mimi niko gado. Nasema hivi mkuu, siku za hao watumiaji madaraka vibaya zimekwisha. Lingoma likivuma sana lakatika. Za mwizi arobaini na kabla ya hapo huwa zinafikishwa kwenye 18 za mwenye sura ya kipole, zikitimia tu wooooote watakwenda na maji hapo. Huyo mama ahesabu siku tu.
Si kweli kama Spika wa Bunge letu hakupeleka salamu za rambirambi. Ni utaratibu mzuri tuliojiwekea kwa Rais, Mawaziri, Wabunge na yeyote anayeguswa na msiba wowote kupeleka salamu za rambirambi, na ndiyo maana vyombo vya habari vikiwemo magazeti, redio, TV zote zilishiriki kikamilifu kwa hilo!
Si vibaya kweli kuungana na wawe wakweli katika kuungana huko na isiwe maneno tu na vitendo vinatakiwa ili tupige hatua mbele katika maendeleo na macho ya wananchi waliowaweka madarakani/bungeni yako wazi yanawatazama. Wananchi wanahitaji watu wakujitolea kwa lilaahi katika kufanya kazi za umma...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.