Makampuni ya simu lazima yalaumiwe maana yanaonyesha hakuna anayefatilia hawa watu wanaosajili namba mtaani unaweza kusajili bila hata kitambulisho au ukamsajilia mtu ilimradi yeye kauza line. Inatokana na uzimamizi mbuvo wa kampuni inayokuwa imempa uagent.
Siku hizi nikipiga huduma kwa wateja najibiwa muda wangu wakupata huduma bule umeisha napewa namba yakupiga na kulipia ndo wanisikilize alafu wameweka matangazo yao unasikiliza mitangazo yao hadi kero hadi upokelewe usaidiwe na elfu 2 inakuwa imeisha. Wananikera na huduma zao basi tu sina lakufanya.
Hali ishakuwa tete kwelikweli kama ndo mtindo wa Helmet hii kiboko.! Inamaana ATM zinakuwa hazina maaskari.? Au wanashilikiana.? Wanaruhusu vipi mtu anaingia kwenye ATM na helmet.?????!!!! Haya maajabu mengine.
Nimesikitishwa na mambo yanayoendelea kwa haya makampuni ya simu katika huduma ya Tigo Pesa na Mpesa pia ATM. Najiuliza ipi sehemu salama yakuifadh pesa.!!!!! Usiku wa kuamkia jumatatu ndugu yangu alitekwa akapewa madawa ya kulevya akaibiwa kila kitu simu, mkoba wake ndani kulikuwa na ATM card...
Ukitokea hidery plaza, oryx shell kabla ya kukutana na barabara kubwa ya kuingia posta mpya pale kuna mashimo miaka nenda rudi hata kabla ya mvua nilishijiuliza maswali mengi sana bila yakupata majibu. Au ile barabara sio ya jiji.!!!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.