Kwanza kabisa tunakushukuru kwa taarifa hii na kukupongeza kwa kuonyesha uzalendo na kuthamini ulipaji wa kodi.TRA tumechukua taarifa hii kwa uzito wa kipekee na tunaenda fanyia kazi mara moja.Ni kosa kisheria kutowasilisha makato ya kodi katika mshahara na pia kuwa na vileo visivyokuwa na stika...
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inawakarabisha wananchi wote kutembelea banda letu katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa 2024 utakaofanyika katika viwanja vya Chuo kikuu cha Ushirika wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro tarehe 2/4/2024.
Aidha TRA itaendelea kutoa elimu ya kodi...
Tumepokea lalamiko hili na tutalifanyia uchunguzi na ikibainika muhusika atachukuliwa hatua kali za kisheria.TRA tunatoa wito kwa wafanyabiashara wote nchini mnapotembelea ofisi zetu kamwe msikubali toa pesa ili mpate huduma kwani huduma tunazotoa ni bure hazina garama yoyote ile.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwataarifu wafanyabiashara wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa katika kipindi hiki cha makadirio ya kodi ya mapato imesogeza Huduma ya makadirio na kupewa namba ya Malipo (control Number) katika vituo vyake vya Huduma kama ifuatavyo
Ilala : Kitunda karibu na...
Mlipakodi anatakiwa kulipa kodi ya mapato kulingana na kile anachokipata. Na kwenye kutafuta kile alichopata tunachukua mauzo tunatoa na gharama za kuendeshea shughuli yake ya uchumi. Muhimu ni kwa kila anachonunua kuwe na risiti ya EFD inayothibitisha manunuzi yake. Pia atatoa gharama zingine...
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tumepokea na kuchukulia suala hili kwa namna ya kipekee na kuahidi kulifanyia kazi mara moja. Aidha tunawakumbusha wadau wetu na walipakodi kuwa endapo watakutana na changamoto yoyote wasisite kuwaona Mameneja wetu wa Mikoa au kuwasiliana kwa namba zetu za bure...
Tunaendelea kuboresha huduma kwa walipakodi na kuongeza uadilifu kwa watumishi wetu wa TRA. Na kuhusu suala la Katavi tunaendelea kulishughulikia kama alivyosema meneja wa Mkoa wa Katavi. Msisite kutoa maoni yenu kwenye semina, mikutano, vipindi vya redio na TV, kupiga simu 0800780078/0800750075...
Mfumo wa IQS unatumika kujibu wateja pale kunapokuwa na uhitaji wa taarifa za ziada ili kuweza kufanya uthaminishaji wa mzigo husika. Wateja wengi wamekuwa hawaangalii taarifa walizoombwa kwenye iqs mapema na kutoa majibu kwa wakati.
Wateja wengi wanaokuja kufuatilia kadhia zao ni wale...
Asante kwa Taarifa ambayo tumeichukulia kwa uzito mkubwa sana na tunaifanyia kazi. Tunapenda kuwaomba wananchi ushirikiano hasa wanapoona taratibu hazipo sawa wasisite kutoa taarifa WhatsApp: +255 744 233333,namba za simu bure kituo chetu cha huduma 0800 750075 au 0800 780078,ukiukwaji wa...
Stempu za kielektroniki za kodi (ETS) zinabandikwa kwenye bidhaa za sigara, maji, juice, bia, mvinyo, soda, CD na DVD. Hivyo siyo kila bidhaa zinatozwa ni zile tu zilizotajwa kwenye sheria ya ushuru wa bidhaa (Excise Duty Act). Na stempu za kielektroniki zipo za karatasi au alama kama...
Asante kwa swali.
Stika hizi za kieletroniki zinaashiria kuwa bidhaa hiyo imelipiwa au inalipa kodi ya ushuru wa bidhaa. Kazi kubwa ya stika hizi ni kutambua kama kodi hiyo imelipwa au italipwa.Na siyo kwa bidhaa zinazozalishwa ndani tu hata zinazotoka nje ya nchi. Mfano sigara au pombe. Ukitaka...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.