Na wakasema hawataki tena rais mwenye historia ya umasikini kama MAGU!!! Walisema magu anafukuza wawekezaji,
Mwaka 2015 rostam alikimbilia Kenya, wakaanza na maneno amekimbiza wawekezaji!!!
Shida ni Imani ya mtu, ni sawa na wale wanaosali novena, huku wengine hiyo nevena hawaiamini kabsa, unamsalia mtu albadir wakati haamini hiyo kitu, itampataje??!
Ukifuatilia matendo ya Hawa wa kuitwa "waaminio Mungu sana" tena hasa kwa kuamini Mungu atatenda baya kwa familia Fulani Ili familia Fulani nyingine ipate raha, utastaajabu mno!!!
Kambona aliombea Nyerere kufa, maalim seif alimuombea Nyerere, cuf wakamuombea mkapa, akina slaa wakamuombea...
Huyo Mungu yeye hajui kuwa mtu anayemuweka atakuwaje?!! Acheni kumsingizia Mungu kwenye kila upumbavu!!!
Kwamba hakuna mikono na akili ya kufanya jambo ni mpaka Mungu aue??! Je akifa ndo solutions??! Nani hafi bhana!!! Yeye unayemuombea mwenyewe anajua lazma afe, na anajua kufa sio lazma wewe...
Tanzania kila mtu amechanganyikiwa na mbaya zaid hakuna anayejua kuwa kuchanganyikiwa!!!
Kifo hakijawahi kuwa solutions ya shida nyingi zetu, ndo maana vitani watu wanakufa na wengine wanakuja kuendeleza!!!
Kutegemea kifo kuwa solutions ndo Ile ya magu mara akaja mama, naye wanaombea afe...
Kutwaliwa, kutwa kutwaliwa, dakika Moja mbele hujui linalokukuta, unatwaliwa wewe, na hujui kama umetwaliwa!!! Na hujui kuwa, wish yako ilikuwa wengine watwaliwe ila sio wewe
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.