Natamani kujua chanzo cha habari hii! lakini hata hivyo kaulimbiu pamoja na kukubaliwa na chama kwamba itumike, kwa kawaida ni pendekezo la mgombea! Utakumbuka katika kipindi kile cha watangaza nia lukuki, tulikuwa na kauli mbiu lukuki! Kuhusu ilani ya uchaguzi, ikiwa ni kweli itabadilishwa na...
Nimejizuia kwa mengi, lakini kwa hili bora niseme nipate amani moyoni! Kwa hatua hii Prof. hukututendea haki! Tutakulaumu hadi dakika ya mwisho, na nakusihi jiandae kupokea tuhuma za "kutumika" kwa manufaaa ya kundi fulani!
Kwa msomi kama wewe, ulipaswa kupima hayo kabla! Umetuingiza mkenge...
Natamani kupata ufafanuzi kuhusiana na suala la pesa linalozungumzwa hapo juu, ni kwamba wamedakishwa mshiko kuusaliti UKAWA au kitu gani?
kwa hujuma sampili hii tutarajie kesho asubuhi, EL akiongea na waandishi wa habari kwamba ameamua kurudi CCM!
Kila mnavyojifanya mnatoa ufafanuzi, mnazidi kumuinua EL. Namshangaa mwanasheria, anajua rushwa imetolewa na kupokelewa kwa viwango alivyovitaja, badala ya kwenda TAKUKURU anakuja humu na blabla nyiiing!!
Nani atakuamini? Tungoje ukweli utajitetea wenyewe!
Wavivu wa kufikiri kama wewe wakiwa vijana, utu uzima ukiwafika hugeuka wachawi! Kama ndugu yangu uko kwenye utu uzima, kaa chonjo, usinga'e Shinyanga! kuna watu wanawashambulia watuhumiwa!
Wewe usiweke kambi popote ili kudukua habari za kiofisi, wewe tinga mtaani kuhamasisha watu kile unachokiamini,Wahamasishe wakuelewe, kisha tukutane kwenye sanduku la kura! Kumbuka usemi wa kiswahili, UDUGU WA NAZI HUKUTANIA CHUNGUNI!! Huu ni wakati wa kutenga ushabiki na harakati za ukombozi!!
Ingawa sijauona mkataba wa makubaliano yaliounda UKAWA, lAKINI NAJUA UKAWA ni makubaliano ya vyama, na wala si muungano wa vyama vinavyounda UKAWA. kwa maana hio kila mwanachama ndani ya UKAWA ana hakisawa na mwenzake,na wala haina maana kwakuwa CHADEMA kinatarajia kuinua mgombea uraisi...
Lugha nzuri katika taarifa yako, lakini kwa kifupi ni kama unapinga CDM kumtumia EL mstari wa mbele katika mapambano ya kuiondoa CCM! Inawezekana uko sawa, lakini, nadhani unajua kila Mtanzania anahamu ya kujua kulitokea nini kule Richmond na kwenye madili makubwa ambayo sisi wagaagaa tunaamini...
Mbona hata hamkusema hayo mapema, wakati makada wakongwe katika Chama lenu walilalamikia mchakato kukiuka taratibu? Tulishuhudia hata wanasiasa makinda wakiwabeza wazee wa fitna katika chama! Hao ndo wajuvi wa fitna zenye majina mengi mazuri ya kuhalalisha maamuzi yao, leo wanajitokeza...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.