Macho kutoa machozi mara kwa mara (Epiphora). Kazi ya macho ni kulainisha, kusafisha na kulinda jicho, ikiwa yatazalishwa mengi au ikiwa kitu kitayazuia kutoka vizuri - kunaweza kuwa na tatizo la macho kutokwa machozi mara kwa mara. Tatizo linaweza kuwa la muda, lakini pia inaweza kuwa ishara ya...
Majeraha yanaweza kupelekea hali isiyo ya kawaida ya Mfupa kujiunda kwenye tishu (Myositis Ossificans) ni hali isiyo ya kawaida ambayo mara nyingi hutokea kwa wanariadha wanaopata jeraha ambalo husababisha kutokwa na damu ndani kwa ndani, kwenye misuli ya ndani. Kutokwa na damu nyingi ndani ya...
Shinikizo la kawaida la damu kwa watu wazima ni 120 kwa 80. Kipimo cha presha hupimwa kwa milimita za zebaki (mercury) (mmHg). Hivyo husomeka kama 120/80 mmHg. Shinikizo la damu hupimwa kwa milimita za zebaki (mmHg) kwa sababu kifaa kinachotumiwa kuipima, kinachoitwa 'mercury sphygmomanometer'...
Video inayoonyesha mtiririko wa damu unaobeba oksijeni na kusambaza katika tishu mbalimbali za mwili, kazi kubwa ya damu ni kusambaza hewa ya oksejeni mwilini. Hewa ya oksejeni huingia mwilini kwa kuvuta pumzi kisha hufika kwenye mapafu na kuingia katika mkondo wa damu na kusambazwa mwilini.
Kipimo cha hesabu kamili ya damu (Full Blood Count) ambacho pia huitwa kipimo kamili cha damu (Complete Blood Count) au kipimo kinachotoa taswira kamili ya hali ya damu (Full Blood Picture) Ni kipimo cha uchunguzi wa damu ambacho hutumika kutoa taarifa muhimu kunako hali ya mgonjwa zinazosaidia...
Kumwaga mbegu kabla ya wakati (Prеmаturе ejaculation) ndio dalili kikuu ya upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume. Ni hali ya mwanaume kushindwa kuchelewesha msimamo wa tendo la ndoa ili kufaidisha na upande wa pili kwa mwenza wake.
Nguvu za kiume hutofautiana kwa mtu mmoja hadi mwingine...
Tatizo la miguu kufa ganzi na kuuma linaweza kusababishwa na hali ya kukaa kwa muda mrefu kupelekea kupunguza mtiririko wa damu au kuweka shinikizo kubwa kwenye mishipa.
Kutetemeka na kufa ganzi kwa muda mrefu au isiyoelezeka kwenye miguu (paresthesia) inaweza kuashiria athari katika mfumo mkuu...
Kondo la uzazi kumtangulia mtoto (Placenta previa) hutokea wakati wa ujauzito, kondo huongezeka ukubwa na kutanuka kadri mfuko wa uzazi unavyotanuka na kukua.
Ni miongoni mwa hali za hatari kwa mama mjamzito ambapo kondo la nyuma hujipachika katika sehemu ya chini ya mfuko wa uzazi, kukua na...
Kifuko cha ujauzito baada ya mimba kutunga (gestational sac) ni muundo uliojaa maji unaozunguka kiinitete (embryo) wakati wa wiki chache za ukuaji wa kiinitete.
Tatizo la Kuyeyuka kwa mimba 'Blighted ovum' hutokea pale ambapo kifuko cha ujauzito (gestational sac) kinakua bila kiinitete...
Sababu zinazopelekea mwanaume kutoa mbegu ambazo zimechanganyika na damu (hematospermia). Sababu inayojulikana zaidi ni kutokana na uchunguzi wa tezi dume (Prostate biopsy) ambapo inahusisha kuondolewa kwa sampuli ndogo za tishu ili kuchunguza saratani ya tezi dumu.
Sababu zisizo za kawaida ni...
Kinyesi cha kawaida huwa na rangi ya hudhurungi (brownish) kutokana na kuwepo kwa kemikali ya 'stercobilinogen' kwenye utumbo. Kinyesi cha watoto wachanga huonekana kahawia-njano au kijani-njano.
Kinyesi Kisicho na rangi (Pale coloured stool) ni kwa sababu ya kukosekana kwa 'stercobilinogen'...
Ngedere hufugwa, ikiwa utamfuga mtu basi tambua yatakayokukuta baadae, lakini ikiwa utaishi na kumuweka kama binaadamu basi kuna faida baadae. Kumbuka ungedere unaujenga wewe na ubinaadamu pia unaujenga wewe, mwanamke ni mtu wa hisia ni lazima ucheze vizuri na hisia zake.
Inatagemea ulimkuta nayo au aliyapata kwako, ikiwa ulimkuta nayo basi ataendelea kujiweka hivyo kwasababu hayo ndio yaliyokuvutia wewe, lakini kama hukumkuta nayo kamwe hawezi kujiweka hivyo kwasababu hayo sio haiba yako.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.