Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, Mkoa wa Pwani, siku ya Jumanne, tarehe 8 mwezi huu, kuwa wafanyakazi 4 wa kampuni ya OYA, walimuua Juma Said Mfaume, wakidai kuwa mkewe huyo Juma Mfaume, anayeitwa Khadija Ramadhan, alikopa pesa toka Kwenye kampuni hiyo ya OYA na akawa harejeshi marejesho...
Hapo umenena Musiba.👏👏
Tatizo la CCM ya kileo ni kuwa hawataki kabisa kukosolewa pale wanapofanya madudu.
Wanachotaka hawa viongozi wa CCM wa kileo ni kusifiwa tu Kwa kwenda mbele.
Hata kama mwanaccm mmoja atamuona mwanaccm mwenzake akiwaibia wananchi, mabilioni ya pesa, akae kimya kabisa...
Kwa kweli suala lililobaki ni kumuomba sana Mungu bila kuchoka ili aonyeshe njia ya namna ya kuondokana na utawala huu dhalimu, uliojikita katika kuwapoteza raia na mauaji holela ya wananchi
Kwa kweli hali inasikitisha sana.
Nakumbuka Rais Samia, baada ya kifo Cha Ali Kibao, ali-post Kwenye ukurasa wake wa Twitter, kuwa amesikitishwa mno na kifo Cha Ali Kibao, hatataka matukio ya aina hiyo yajitokeze nchini kwetu, Kwa kuwa nchi hii ni ya kidemokrasia na Kila mtu ana HAKI ya KUISHI...
Hivi wewe hujui kuwa maandamano ya amani ni halali kufanyika Kwa mujibu wa Katiba ya nchi hii, sasa kulikuwa na sababu zipi Kwa serikali hii ya CCM, kuwakusanya mapolisi wote wa nchi hii kuja Dar Kwa lengo la kuwatisha raia Ili wasiweze kuandamana??😳
Hayo maandamano tuliwaachia hao mapolisi kuandamana Kwa niaba yetu
Wewe kama ni mkazi wa Jiji la Dar, utakubaliana nami, Kwa kuwa uliona namna Polisi wote toka mikoani walivyojaa jijini Dar na kuanza kuandamana wakiwa na silaha za kivita, utadhani nchi yetu ipo vitani, wakiwa na farasi...
Hata Mimi nimekuwa nikijiuliza hivi Kwa mfano huyo Soka, amekuwa tishio Kwa kiasi Gani, Hadi ifikie System, iamue kumteka na asijulikane alipo Hadi hivi sasa??
Hizo hoja wanazotoa hao maccm, naweza kuziita kuwa ni walioishiwa na hoja
Hivi kama kweli sisi wapinzani ndiyo tunaofanya huo utekaji, ni kwanini basi hata huo wito tunaotoa wapinzani wa uundwaji wa Tume huru ya kijaji unaotolewa na vyama vya upinzani, nao unapingwa kutekelezwa na serikali hii...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.