Nguvu ya injini ya kirikuu ni cc 660. Kama unataka kubeba watu kumi bila kumuingiza hasara mwenye gari, tafuta noah kama barabara ni zuri. Kama barabara ni mbaya, tafuta toyota hilux.
Je itakuwa inabeba watu wangapi? Bado najiuliza kwa nini ukodi pick up kwa ajili ya kubeba watu. Mimi ninayo lakini nahitaji majibu ya maswali hayo kabla ya kuamua kukukodisha.
Sasa nimejua tatizo lako. Baada ya kufungua, ulitakiwa uwe unachungulia. Kwa sifa ulizonazo, utakuwa ulichaguliwa NACTE wakasubiri uthibitishe kwenye profile yako haukuthibitisha, hivyo nafasi yako watapewa waliiomba safari ya pili. Nashauri utumie namba za simu ulizopewa, uwapigie NACTE.
Naona kama haueleweki vizuri. Ni bora kuwa wazi ili wanaojua wakufahamishe. Nilikuuliza kama uliomba NACTE kwa kutumia CAS ukasema ndiyo ulitumia. Wakati huo unaomba msaada jinsi ya kutumia. Sasa ulitumiaji kuomba wakati hujui.
Wote walioomba kwa kutumia CAS, kila mtu kwa sasa anaelewa hatma yake. Kama hauelewi, maana yake ni kwamba haujui jinsi ya kuitumia. Itabidi usubiri mwaka kesho.
Taarifa kwa wote mliokwishaconfirm ni kwamba hamna tena haja ya kuingia kwenye profile zenu maana kazi yake imekwisha. Sasa mnatakiwa kuwa mnachungulia e-mail ili kuona kama joining instructions zimetumwa. Wale mliochagua mara ya pili, endeleeni kuchungulia profile zenu.
Hapo nimemuelewa. Kama aliishaconfirm ikaandika yes, sasa kwenye profile anatafuta nini tena? Kazi yake kwenye CAS imeisha sasa awe anachungulia kwenye email yake maana atatumiwa joining instructions ya chuo alichochaguliwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.