Jamani kama una mapenzi na mtu kwa hisia zako, endelea nae mkanywe naye chai. Je wote waliokosa ubunge walimsema Pr. Muhongo. Mbona wapo wengi tu walimsema na wamerudi bungeni. Ilaelekea wewe siyo mfuatiliaji wa mambo, umelipuka tu.
Ndugu yangu Tetty, mgomo unaosema upo sana ni mgomo wa woga na unaangamiza taifa lote. tunataka mgomo wa uzalendo ambao ni mgomo wa wazi ambao unatafuta suluhisho la mapema ili taifa lisiangamie kama mnavyofanya, mgomo wa kimyakimya huo ndio upumbavu na ujinga unaosemwa!
Jamaa uliye Arusha, mbona umetoa kali leo, yaani huyo Mzenji na Mtanganyika wanaweza mchakamchaka, du! Tanzania ya leo haihitaji watu wa kimya kiasi hicho. Tunahitaji kiongozi shupavu ambaye hata ukimtazama anavyoongea, na usoni anaonyesha hivyo!
Viongozi wa Afrika wamezidi kupenda madaraka, wananchi wa Burundi walijua fika wakisubiri sanduku la kura Nkurunzinza atapita tu kwa hila! Nawapongeza wanajeshi wa Burundi ilimradi nao wasiwe kama waliyempindua.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.