Watanzania wa upande wa bara wanaotembelea visiwani wanahisi kubaguliwa na ndugu zao wa Zanzibar kwa kuwa huitwa chogo.(watu wenye mabichwa makubwa🤣)
Wazanzibari hawana mabichwa🤣 kama hayo🤣.
Hili huenda ni utani wa kawaida kama watanzania kwa ujumla wanavyotaniana kutokana makabila yao au maeneo...
Wazanzibari wanalaumu muundo huu wa Muungano unaifaidisha zaidi Tanganyika.
Wanasema Tanganyika imejificha kwenye serikali ya Muungano.
Wanasema kile kinachosemwa mambo muungano ki wizara ni manne ili hali serikali yote pamoja na wizara na taasisi zilizo chini yake ni za Muungano.
Wazanzibari wanasema Muungano wa haki ungekuwa wa serikali tatu ili kila upande usimamie mambo yake na kisha serikali kuu "Central Government" isimamie mambo makubwa
Baadhi ya wazanzibari wanasema kwamba Muungano huu umeingiwa kwa pupa na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar baada ya mapinduzi bila kuwashirikisha wananchi wa pande zote
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.